Thursday 23 July 2015

CHADEMA UBUNGE LUDEWA WAENDELEA KUMWAGA SELA ILI KUMPATA MGOMBEA MMOJA

                                 Wakili Paulo Kalomo mgombea ubunge jimbo la Ludewa


Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilayani Ludewa kimeendeleana na mtifuano mkali katika kumsaka mgombea mmoja wa ubunge wilayani hapa ambapo kila mgombea amekuwa akipita huku na kule kusaka kura kwa wajumbe wa Chama hicho huku baadhi yao wakituhumiana kutumia pesa zaidi.
Akiongea na waandishi wa habari jioni ya leo Wakili Paulo Kalomo ambaye ni miongoni mwa wagombea wa nafasi hiyo akitokea mwambao wa ziwa Nyasa alisema kuwa mpaka sasa kuna wagombea wanne hivyo yeye amekuwa na mvuto zaidi kwa wajumbe hali ambayo inawafanya wagombea wenzake kukata tamaa na kuwarubuni wajumbe.
Wakili Kalomo alisema kuwa akifanikiwa kuchukua nafasi hiyo atakibadirisha chama cha demokrasia na maendeleo wilayani Ludewa kwa kujijenga kuanzia vijijini hadi ngazi ya wilaya hivyo amewataka wajumbe wa chama hicho kutorubuniwa na baadhi ya wagombea katika kura za maoni zinazotarajiwa kupigwa leo tarehe 23/7/2015 katika makao makuu ya wilaya kwani yeye anamipango endelevu kwa wilaya ya Ludewa.

No comments:

Post a Comment