Friday 30 January 2015

Msanii Suge Knight akamatwa kwa mauaji

Suge Knight
Polisi nchini Los Angeles inasema kuwa msanii wa muziki wa rap kutoka Marekani Marion Suge Knight amekamatwa kutokana na mashtaka ya mauaji baada ya kumgonga mtu mmoja na gari lake hadi kumuua na baadaye kutoroka.
Polisi wanasema kuwa bwana Knight alijibizana na watu wawili katika eneo la kuegesha magari na baadaye kumgonga mmoja wao huku mwengine akijeruhiwa vibaya.
Wakili wake anasema ilikuwa ajali na kudai kuwa mteja wake alishambuliwa na watu wawili.
Suge Knight ni mwanzilishi wa kampuni ya Death Row Records ambayo iliwazindua wasanii maarufu wa mziki wa rap akiwemo Snoop Dogg na marehemu Tupac Shakur.

Baba ajiua kutokana na picha za mwanawe

Loredana Chivu ni mwanamitindo nchini Romania
Baba mmoja amejiua baada ya kuona picha za uchi zamwanawe wa kike katika jarida la Playboy nchini Romania.
Loredana Chivu alirarua ukurasa uliokuwa na picha yake akiwa 'amepos' katika jarida hilo la Playboy na punde babake alipogundua kuhusu picha hizo, alizongwa na mawazo na hata kumkana mwanawe.
Kwa mujibu wa mtandao wa Mirror, msichana huyo mwenye umbo la kuvutia alisema, '' babangu aliacha kuongea na mimi na kuonekana mwenye hasira sana''.
"alipogundua kuwa picha hizo zilikua zangu, alijitenga sana na kujaribu kunitenga na mimi''.
Nilidhani labda angesahau na sikudhani hata siku moja angejitoa uhai.
Loredana Chivu anasema anajuta sana kwani babake hakuwahi kuongea naye baada ya kupata picha zake
Mwanamitindo huyo Loredana Chivu mwenye mamia ya picha akiwa nusu uchi kwenye akaunti yake ya Instagram, alikuwa na uhusiano wa karibu sana na babake lakini alisema yote hayo yalibadilika baada ya babake kuona picha zake akiwa nusu uchi.
Alipokwenda kumtembelea babake miezi michache baadaye, baada ya kuamua kwamba kimya kilikuwa kimeendelea kwa muda mrefu sana, alishtuka sana kumpata babake akiwa amejitoa uhai
"nilipata akiwa na kamba shingoni akiwa ananing'inia chumbani''.
Loredana,anayeishi nchini Romania, anasema kuwa tangu kifo cha babake, amekuwa akiwaza na kuwazua kwamba aliamua kujiua kwa sababu ya mgogoro kati yetu na hasa kuhusu picha zangu zilizoziona kwenye jarida la Playboy.
''Najuta sana kwamba hakuwahi kupata muda wa kuzungumza na babangu kuhusu yaliyotokea''.
''Hakuwacha ujumbe wowote kabla ya kujitoa uhai, siku zote tulikuwa na uhusiano mzuri lakini yote yalibadilika baada ya baba kuona picha zangu nikiwa uchi. Bado inaniuma sana na singemtakia mtu yeyote kupatwa na kama yaliyonikuta''.

ANGALIA PICHA- BIBI ANAYEDHANIWA KUWA MCHAWI AKUTWA AKIWA UCHI..CHEKI TUKIO LOTE HAPA

Hatimaye bibi akaweza kusimama na kuanza kufanya vituko vya kila aina
-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

Bibi akaamua kukaa na kuanza kutoa pesa alizokuwa amezifunga kiunoni kwa kwenye mfuko mlaini-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

Zilikuwa ni shilingi za hamsini hamsini,mia moja ,mia mbili,mia tano na elfu akaziweka kwenye kibakuli kilichokuwa eneo la tukio
-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

Kushoto ni mjumbe wa serikali ya mtaa wa Mageuzi Waziri Musa(CHADEMA) akisaidiana na wananchi wa eneo hilo kumwondoa bibi huyo kwenye nyumba ya mkazi wa eneo hilo
-picha na Kadama Malunde-Shinyanga



Bibi akiwa amelala juu ya mawe kabla askari polisi hawajafika eneo la tukio leo mchana japokuwa bibi huyo amekutwa nyumbani kwa mtu saa moja asubuhi-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

Askari polisi wakimwangalia bibi huyo
-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

Askari polisi wakitoa maelekezo kwa wananchi wa mtaa huo ambapo walisema serikali haiamini ushirikina hivyo kuwataka wananchi waondoke eneo la tukio na kumwacha bibi aendelee na safari yake kwani tayari alikuwa ameanza kutembea
-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

Askari polisi akiwa amembeba bibi huyo kumtoa kwenye mawe,na katika hali ya kushangaza bibi huyo alimng'ang'ania askari huyo-picha na Kadama Malunde-Shinyanga

TOA MAONI YAKO HAPA

HUU NDIO UKWELI KUHUSU TEVEZ ALIYEKATWA UUME WAKE BAADA YA KUWADHULUMU MADAWA YA KULEVYA WENZAKE

HABARI ZA UHAKIKA JUU YA SAKATA LA JUMAANNE TEVEZ. Nikweli kwamba huyu bwana yuko South Africa Pretoria. Bwana Tevez alodhaminiwa mzigo na vijana wenzake huko Bondeni kwamba akauze kisha alete Mpunga. Mdhamini alikuwa ni Kijana wa Kibongo anayeonekana pichani anayeitwa Jeff Katili mtoto wa Ilala ambaye maskani yake ni South. TEVEZ baada ya kuchukua mzigo uliokuwa na thamani ya takriban milioni mia moja na hamsini (150,000,000/=) aliingia mitini hakurudi tena. Kilichotokea Jeff baada ya kubanwa na wana akawaambia kuwa tulieni nitamleta tu.

 Basi Jeff akamrubuni Tevez kuwa njoo Kuna kazi.. Tevez akaingia mzima mzima akaenda hadi Pretoria wiki iliyopita na kufikia kwa Jeff Katili na kupata mapokezi mazuri kama kawaida. Baada ya kufika walitoka kwenda matembezi KWAZULU NATAL... wakiwa huko walifikia kwa washkaji zao wa kibongo lakini kwenye nyumba ambayo ilikuwa kama holi haina chochote ndani. Chini lilitandikwa karatasi la nailoni ili kuepusha damu isitapakae. Alibanwa juu ya mzigo na mtesaji mkubwa alikuwa Jeff Katili mwenyewe ambaye ni mdhamini. Tevez hajang'olewa jicho bali alipigwa Ngumi hadi jicho likaenda ndani... NGUMI YA MTOTO WA KIUME.

Ameteswa sana na amekatwakatwa na viwembe mwili mzima. Zakari yake haijakatwa kama picha zilivyoonyesha bali imekatwa na viwembe. Taarifa zilitumwa kwa kaka yake na akina Jeff na kuwataka watume pesa la sivyo wanamuua. familia kupitia kaka yake imeshatuma pesa nusu na sas anatibiwa hukohuko South na atarejea punde. Uzushi kuwa amekufa hauna ukweli na hizi ni habari kamili kutoka kwa watu wa karibu na familia hiyo.
Chanzo cha Habari ni msamablog.com

TOA MAONI YAKO HAPA