Wednesday 26 November 2014

THIS IS TOMUCH! SASA SAKATA LA MTOTO WA MIEZI 6 ALIYEFIA MAHABUSU MAPYA YAIBUKA..SOMA HAPA TUKIO ZIMA

mtotozi
LILE sakata la mtoto wa miezi 6 (pichani) kufia mahabusu ya Kituo cha Polisi cha Kova, Mbezi Kwamsuguri, Dar linaendelea! Safari hii, mama wa mtoto huyo, Meradi Meshack  ameibua mazito akiwataja polisi jamii kuwa ndiyo chanzo cha kifo cha mwanaye.Ψ
Awali ilibainika kuwa, mtoto huyo aliyefariki dunia Novemba 18, mwaka huu wakati mama yake akiwa amewekwa kituoni hapo kama mhalifu, polisi wa kituo hicho walitajwa kuhusika.
Akizungumza na waandishi wetu, mama huyo alisema  yeye na mtuhumiwa wake aliyemtaja kwa jina la mama Na walikuwa wakidaiana fedha za upatu ambazo alikuwa akimdanganya kuwa wanachama wenzake bado hawajatoa.
Baada ya usumbufu wa muda mrefu ndipo wakapishana maneno, mwanamke huyo akampeleka polisi akidai alitaka kumpiga. “Nilifuatwa na polisi jamii wawili na si polisi wenyewe. Mimi nilikuwa na mume wangu, niliwaambia mwanangu anaumwa nitakwenda kesho lakini hawakukubali, wakanitukana na kunichukua kwa mabavu huku mwanangu akiwa na hali mbaya na walimuona..
“Shangazi yangu na mume wangu walinifuata wakitaka kuniwekea dhamana, wale polisi jamii wakakataa, wakanitupa mahabusu. Mwanangu akazidi kuwa na hali mbaya zaidi maana hali ya hewa mle mahabusu ilikuwa ni nzito sana.
“Usiku nilipitiwa na usingizi, niliposhituka usiku wa manane nikamuona akikohoa na kupumua kwa shida, baadaye akalegea na kuwa kama amelala, nikawaita wale polisi jamii lakini hawakuja. “Ndipo alfajiri, mmoja wao akaja, akanitazama kisha akaondoka zake. Akaja mwingine, akamshika mwanangu  akawa kama ameshtuka, akaniambia niondoke haraka nimpeleke hospitali
“Kumbe wakati anasema hivyo alishajua mwanangu amefariki dunia, inauma sana kwa kweli! Nilitoka na kilio kwani nilishampoteza mtoto wangu na wao sikuwaona tena! Walikimbia! Huu ni ukatili wa hali ya juu,” alisema mwanamke huyo.
Naye mjumbe wa eneo hilo, Rashid Sultan alisema taarifa za kifo cha mtoto huyo alizipata na kuwatupia lawama polisi jamii waliojichukulia uamuzi wa kumweka mahabusu mwanamke huyo tena akiwa na mtoto mchanga wakati kituo hicho ni kidogo na hakilazi wahalifu nyakati za usiku na hutakiwa kufungwa saa 12 jioni.
Inadaiwa kuwa, chanzo cha mtoto huyo kufariki dunia ni kukosa hewa huku akiwa anasumbuliwa na kifua. Hadi Uwazi linakwenda mitamboni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura hakuwa akipatikana kwenye simu yake ya mkononi ili kuelekeza anachokijua.
Marehemu alizikwa Novemba 19, mwaka huu kwenye Makaburi ya Mbezi Kwamsuguri jijini Dar. Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.