Wednesday 22 July 2015

ZAIDI YA WAZEE 300 WAMCHANGIA NA KUMCHUKULIA FOMU YA UBUNGE FILIKUNJOMBE JIMBO LA LUDEWA. Wasema wameridhika na utendaji wake.

 Baadhi ya wazee wa wilaya ya Ludewa wakimpa baraka za mwisho za kuanza kugombea kwa awamu ya pili Mh.Deo Filikunjombe
Filikunjombe akisikiliza nasaha za Wazee

 msafara wa kumsikindikiza kutangaza nia ya kugombea ubunge Deo Filikunjombe ukiingia viwanja vya mpira wa miguu Ludewa mjini
Filikunjombe akiwasalimia mamia ya wanachama wa ccm wilayani Ludewa ambao walikuja kumuunga mkono

wasanii wa kikundi cha IVA YOUTH GROUP ambacho ni kikundi cha uhamasishaji wilayani hapa wakifanya yaliyo yao
                                       mamia ya washabiki wa ccm wakimraki Filikunjombe


Filikunjombe akiongea na wananchi wa wilaya ya Ludewa kata ya Ludewa mjini wakati akitangaza nia ya kugombea ubunge

                   msanii wa IVA youth Group Seleman Chikuti akionesha umahiri wake katika sanaa
 Seleman Chikuti toka kundi la IVA youth group linalopatikana Ludewa mjini akifanya vitu vyake wakati Deo Filikunjombe akitangaza rasmi nia ya kugombea ubunge wa jimbo la Ludewa







Zaidi ya Wazee 300 wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wamefanya

maandamano ya kumuunga mkono mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo

Filikunjombe na kumchukulia fomu ya kugombea nafasi ya ubunge wa

jimbo hilo kwa awamu ya pili ili aweze kuliongoza tena kwa kauli ya

kuwa wameridhishwa na utendaji wake ambao hauna mashaka.


Akizungumza kwa niamba ya wazee wenzake mzee Laurent Mtweve alisema

kuwa jimbo la Ludewa limekuwa na umaarufu mkubwa wa kubadili

wabunge kila baada ya miaka mitano kutokana na utendaji

usioridhisha lakini safari hii hakuna haja tena ya kufanya hivyo

kutokana na mafanikio makubwa yaliyofanyika katika kipindi cha

Filikunjombe.


Mzee Mtweve alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2010 HADI 2015

wilaya ya Ludewa imepata mabadiriko makubwa katika kila sekta kwani

wakati mwingine Filikunjombe hakuweza kuisubiri bajeti ya Serikali

alilazimika kutoa fedha za posho yake ili kufanikisha na kutatua

matatizo yanayowakabiri wananchi wake.


Naye Bi.Mariam Nyandoa alisema kuwa katika moja ya kazi ambayo

Filikunjombe anapaswa kuendelea na uongozi ni ile ya kuhakikisha

kila hospitari,zahanati,dispensari kunakuwa na watumishi pamoja na

vitanda vya kujifungulia hali ambayo imekuwa ni kilio cha wanawake

wilayami Ludewa kwa muda mrefu.


Bi.Mariam alisema kuwa kwa sasa hakuna shida tena kama ilivyokuwa

awali kwani unapokwenda hospitari unauhakika wa kupata huduma nzuri

hivyo wazee wote wakaona wachange fedha za kumchukulia fomu ya

kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Ludewa na pia wanaandaa

sherehe ya kumpongeza kwa uongozi wake mzuri ambao ameuonesha.


"Sisi kama wazee katufanyia mengi katika kipindi cha uongozi wake

na yamekuwa ya mafanikio kwa wilaya ya Ludewa kumpata mbunge kijana

na ambaye anatumika akitumwa hivyo tunampango wa kumfanyia sherehe

licha ya kuwa tumemchukulia fomu hivyo hatuna mpango wa kuwa na

mbunge mwingine zaidi yake",alisema Bi.Nyandoa.


Akiongea na umati wa wananchi wa wilaya ya Ludewa katika viwanja

vya michezo Ludewa Mjini wakati akitangaza nia ya kungombea nafasi

ya ubunge Mh.Deo Filikunjombe alisema kuwa mafanikio yote

yaliyopatikana sio juhudi zake binafsi bali ni ushirikiano

alioupata toka kwa wananchi wa jimbo lake.


Filikunjombe alisema kuwa katika kipindi cha uongozi wake ni kweli

kumekuwa na mafanikio makubwa lakini wananchi ndio waliokuwa

wakimsukuma kufanya hayo na wakati mwingine alikuwa mkali Bungeni

kutokana na halia halisi ya ugumu wa maisha ya wananchi wa wilaya

ya Ludewa.


Alisema kuwa anamshukuru rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kwa

kuitendea haki wilaya ya Ludewa kwani katika kipindi cha uongozi wa

ke Ludewa imekuwa ikisikilizwa kupitia yeye hali ambayo

imeharakisha maendeleo wilayani Ludewa.


Anasema katika ubunge wake wa miaka mitano Ludewa imeweza kupata

kipande cha lami na hatimaye barabara za mitaa ya Ludewa mjini

zimeweza kung'ara kwa lami ikiwa ni juhudi zake kwani kabla ya

kuingia katika ubunge wilaya ya Ludewa haikuwa hata na kipande

kimoja cha lami.


Alisema kuwa licha ya Lami lakini barabara za vijijini vimefunguka

mfano barabara ya Lupingu ambapo kwa sasa kuna gari za abiria

zinafika huko wakati awali haikuwezekana pia barabara ya Mawengi

makonde ambako kwa sasa samaki wabichi wa ziwa nyasa wanafika

mapema Ludewa mjini.


Pia katika nishati ya umeme alivikuta vijiji vitatu vta

Mavanga,Mawengi na Ludewa mjini ndivyo vilikuwa na umeme lakini kwa

sasa kunamiradi ya umeme katika vijiji 67 ikiwa wilaya ya Ludewa

inajumla ya vijiji 77 hivyo anatangaza nia ya kugombea tena nafasi

hiyo ili aweze kukamilisha vijiji vilivyobaki.


Filikunjombe alibainisha kuwa wilaya ya Ludewa inatakiwa

kubadirishwa haraka na haya machache ambayo wananchi wanayaona kama

ni mabadiriko makubwa kwake ni machache sana kwani Ludewa imekuwa

nyuma kimaendeleo kwa miaka mingi hivyo katika mipango yake ya

ujenzi wa lami barabara kuu tayari Serikali imeshatoa fedha ya

kujenga barabara hiyo na awamu ya kwanza itajengo kilomita 50.


Alisema ujenzi wa barabara hiyo unaanza mapema mwezi ujao ambapo

Dkt.John Pombe Magufuli atakuja kabla ya kuanza ujenzi ili kujionea

mafanikio aliyoyafanya kwa wananchi wa wilaya ya Ludewa katika

sekta ya miundombinu na baadaye atakuja Rais Dkt.Kikwete kuweka

jiwe la msingi la ujenzi wa viwanda vya chuma cha Liganga na makaa

ya mawe Nchuchuma.


Aliwataka wananchi wa wilaya ya Ludewa kumuunga mkono mgombea wa

nafasi ya urais kupitia chama cha mapinduzi Dkt.Magufuli kwani ni

kiongozi makini na anayeipenda wilaya ya Ludewa kwa ni bila yeye

hata barabara za lami wilayani hapa tusingezipata hivyo wananchi wa

wilaya ya Ludewa wanahaki ya kujivunia kwa kuteuliwa Dkt Magufuli.


Filikunjombe alisema kuwa hivi sasa Serikali imepitisha bajeti ya

ujenzi wa daraja la mto ruhuhu ili kuunganisha wialaya ya Ludewa na

ile ya Nyasa hivyo wananchi wanatakiwa kujiandaa na fulsa ya

kibiashara watakayoweza kufanya na mkoa jirani wa Ruvuma.


Mwisho. 

Habari na: http://habariludewa.blogspot.com

Wabunge Chadema waangukia katika kura za maoni


Wanachama wa Chadema wilaya ya Mbeya Vijijini
Wanachama wa Chadema wilaya ya Mbeya Vijijini wakitoka nje ya ukumbi baada ya msimamizi wa uchaguzi wa kura za maoni za kumpata mgombea ubunge jimbo la Mbeya Vijijni kutokomea kusikojulikana  wakati wa kuhesabu kura jana na kusababisha uchaguzi huo kuvunjika. Picha na Godfrey Kahango 
By Waandishi Wetu, Mwananchi
Dar/mikoani. Kura za maoni ndani ya Chadema zimeanza kuwa chungu kwa baadhi ya wabunge. Mbunge wa Mbulu, Mustapha Akoonay na mwingine wa Viti Maalumu, Susan Lyimo (Kinondoni) jana waliangukia pua, huku mwenzao wa Karatu, Mchungaji Israel Natse akitangaza kuachana na ubunge na kurejea katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).
“Jumatano (leo), nitawaaga rasmi wananchi wangu, binafsi niliombwa na Dk (Willibrod) Slaa kugombea jimbo hili kwa miaka mitano,” alisema.
Lyimo alianguka baada ya kupata kura 32 nyuma ya Mustafa Muro aliyepata kura 47. Wengine ni Rose Moshi (8), Agrey Mkwama (6), Gemeral Kaduma (4) na Francis Nyerere (0). Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa alisema tayari uchaguzi umefanyika katika majimbo matano.
Alisema Mbulu Mjini, kulikuwa na wagombea wawili, Akoonay alipata kura 108 dhidi ya 132 alizopata Diwani wa Mbulu, Michael Sulle.
Golugwa alisema, Joseph Selasini ametetea nafasi yake katika Jimbo la Rombo baada ya kupata kura 313 akiwaacha mbali wapinzani wake Ben Sanane aliyepata kura 26 na wengine kura mojamoja.
Babati Mjini, Mbunge wa Viti Maalumu, Paulina Gekur ameibuka kidedea kwa kura 88 akiwatupa nje wapinzani wake, akiwamo mkuu wa wilaya wa zamani, Gabriel Kimolo na wenzake.
Mbulu Vijijini, Aman Gaseri alishinda kwa kura 76 huku Michael Aweda akipata 75.
Jimbo la Same Magharibi: Jonas Kadeghe alishinda kwa kura 68 akifuatiwa na Christ Mbanjo aliyepata kura 49 na Gervas Mgonja kura 30.
Muleba Kaskazini: Najim Kasange alipata kura 247 na kumshinda mwandishi wa habari mkongwe, Ansbert Ngurumo aliyepata kura 55. Mgombea mwingine, Christina Mwainunu alijitoa.
Jimbo la Ukonga, Nickson Tugara alishinda kwa kura 59 hivyo kuwaacha kwa mbali wagombea wenzake 14. Alifuatiwa na Waitara Mwikwabe aliyepata kura 49, Elly Dallas (15), Deogratias Munishi (8), Lucas Otieno (6), Asia Msangi na Deogratias Mramba waliopata kura tano kila mmoja na Gasto Makwetta (1). Wengine saba hawakuambulia kura hata moja.
Butiama: Yusuf Kazi aliibuka kifua mbele baada ya kujikusanyia kura 202 na kuwapiku Adam Taya (39) na Issa Yusuf (31), Daniel Obeiya (3), Annicent Marwa (2) na Lucas Ossoo na Marto Yohana waliopata kura moja kila mmoja.           
  Nyamagana: Wenje aliibuka kidedea kwa kupata kura 194 na Patrick Masagati (32).
Msalala: Paulo Ndundi alishinda kwa kura 113 akiwashinda Peter Machanga (49) na Ezekiel Kazimoto (48). Wengine ni Emmanuel Mbise (43), Francis Makune (15), Vincent Manoni Mhagwa (10) na Richard Mabilika aliyepata kura moja na Stephen Bundala (0).
Sumbawanga: Shadrack Malila aliibuka na ushindi wa kura 277 dhidi ya Kassian Kaegele (28), Musa Ndile (9) na Matokeo Lyimo (1), Eliud Mwasenga na James Kusula (0).
Nkasi Kusini: Alfred Sotoka aliongoza kwa kupata kura 70 akifuatiwa na Kaminga Hyporito (39), Emmanuel Sungura (9), Edson Ndasi (4) na Joseph Kitakwa (2).
Nkasi Kaskazini: Keissy Sudi alishinda kwa kura 158 na kufuatiwa na Triphone Simba (70) na Stanley Khamsini (5).
Kwela: Daniel Ngogo aliwabwaga wenzake kwa kura 151 akifuatiwa na James Mwamlyela (117), Ameri Nkulu (27), Alstidi Maufi (13) na Michael Moka (4).
Mlalo: Kelvin Shemboko alipata kura 56 akifuatiwa na Lewis Kopwe (31), Jumanne Pazia (15) na Mkazeni Mkazeni (0).
Mabadiliko ya ratiba
Wakati kukiwa na sintofahamu na wanachama wanaojiunga na Chadema huku kipindi cha kurejesha kikiwa kimekwisha, chama hicho kimetangaza mabadiliko kwenye ratiba ya kurudisha fomu hasa katika majimbo mapya yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Julai 12.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika alisema jana: “Fomu za kugombea kwenye majimbo hayo zitaendelea kutolewa na hata kura ya maoni watapiga tofauti na majimbo yaliyokuwapo.”
Alisema hata katika majimbo mengine, Sikukuu ya Eid el Fitr iliingilia ratiba iliyopangwa awali na kwamba uongozi wa chama umeona kuwa ipo haja ya kuongeza siku ili kutenda haki kwa wale waliokosa kulipia fomu benki kutokana na sherehe hizo.
“Kinachotakiwa sasa ni katibu wa wilaya kutuma mapendekezo ya kuongeza siku atakazoona zitafaa kwa zoezi hilo na makao makuu itaidhinisha hilo,” aliongeza.
Msimamizi ‘aingia mitini’
Uchaguzi wa mgombea ubunge Mbeya Vijijini ulikwama baada ya msimamizi wa kura za maoni wa Chadema, Christopher Mwamsiku kutokomea kusikojulikana katika hatua za mwisho.
Kitendo hicho kiliwafanya wajumbe wa Kamati ya Siasa Mbeya Vijijini na mawakala kubaki njiapanda wasijue cha kufanya huku wengine wakidai kuwa hizo ni njama za kutaka kumbeba mmoja wa wagombea.
Mwenyekiti wa Chadema wilayani hapo, Jackson Mwasenga alishindwa kutoa maelezo ya tukio hilo huku akimtaka katibu wake kuzungumza.
Katibu huyo, James Mpalaza alisema: “Hata sisi hapa kama unavyotuona tumeduwaa hatujui ni kwa nini ameondoka.”
Alipotafutwa kwa simu, Mwamsiku alijibu kwa kifupi: “Sijakimbia, nimeondoka kwa utaratibu mzuri tu… lakini siwezi kukwambia ni kwa nini kamuulize Mwasenga anayo majibu yote niache nipumzike.”
Dalili za kuvurugika kwa uchaguzi huo zilianza wakati wa kuhesabu kura baada ya Mwenyekiti wa Bavicha, Mbeya Vijijini kuingia ndani ya chumba hicho akidaiwa hahusiki jambo lililozua mzozo mkubwa uliodumu kwa takriban dakika tano hadi alipotoka.
Wengine wajitokeza Chadema
Tabora Mjini: Peter Mkufya, Nhombar Imajamasallah, Elifuraha Kisangi, Said Mwakasekela na Raymond Maganga.
Kaliua: Anthony Mwakammoja, Godluck Jilinga, Prosper Guga, Peter Msazya na Wilson Lukobe.
Ulyankulu:  Dk Deus Kitapondya.
Igalula: Mustapha Kado na James Kabepele.
Tabora Kaskazini: Daud Nteminyanda.
Igunga: Joseph Kashindye, Ngasa Mbojenamba na Gw’igulu Darushi.
Manonga: Ally Halfan Nguzo, Athanas Shija Michael na Simon Seleli.
Nzega Vijijini: Albino Mayani Simbila na Nicholaus Zakaria.
Nzega Mjini: Gisberth Kabamba, Daniel Simba, Boniface Masasi, Charles Mabula, Monica Nsaro, Ally Ndee na Mary Atonga.
Bukene: Alex Mpugi, Lumola Kahumbi, Elias Machibya, Dickson Kagembe na Emmanuel Ntobi.
Rorya): Mtatiro Sanya, Evangel Dea, Kevin Makooko, Matiko Seruka, Emmanuel Werema, Ezekiel Kachare, Steven Owawa, Opiyo Nalo, Herman Odemba,  Thomas Risa na  Ochora Ndira.
Tarime Vijijini: John Heche, Peter Busene, Moses Yomami, Prosper Nyamuhanga, Johanes Manko na Fabiani Mwita.
Tarime Mjini:  Ester Matiko, Lucas Ngoto, Christopher Chomete, Charles Werema na Martinus Joseph.
Waliojitokeza CCM
Arumeru Mashariki: Elirehema Kaaya, Jackson Ezekiel, John Sakaya. Angela Palangyo, William Sarakikya, Dk Daniel Pallangyo na Siyoi Sumari.
Longido: Philip Kitesho, Dk Stivin Kiluswa, Lee Mamaseta, Daniel Marari, Lesioni Mollel, Joseph Kulunju, Lemayani Logoliye na Emmanuel Sirikwa.
Monduli: Sakata Babuti, Loota Sanare, Loliayu Mkoosi, Namelock Sokoine, Mbayani Kayai na Amani Turongei.
Arumeru Magharibi: Loy Thomas Sabaya, Daudi Mollel, Elisa Mollel, Osilili Losai, Henri Majola, Lekoko Piniel na Lomoni Mollel.
Ngorongoro: Eliaman Laltaika, Elias Ngolisa, Joseph Parsambei, Patrick Kasongo, William Ole Nasha na Saning’o Telele.
Karatu: John Dodo, Dk Willbrod Rorri, Joshua Mbwambo na Rajabu Malewa.
Arusha Mjini: Mustapha Panju, Justin Nyari, Philemon Mollel, Victa Njau, Thomas Munisi, Hamis Migire, Admund Ngemera, Moses Mwizarubi, Ruben Mwikeni, Endrew Lymo, Salehe Kiluvia, Lukiza Makubo, Mohammed Omar na Emmanuel ole Ngoto.
Mkalama: Mgana Msindai, Profesa Shaban Mbogho, Nakey Sule, Orgenes Joseph Mbasha na Allan Kiula, Emmanuel Mkumbo, Dk Kissui Kissui, William Makali, Kyuza Kitundu, Dk Charels Mgana, Salaome Mwambu, Francis Mtinga, Dk George Mkoma na Lameck Itungi.
Manyoni Magharibi: John Lwanji, Eliphas Lwanji, Jamal Kuwingwa, Jane Likuda, Mohammed Makwaya, Yahaya Masare, Athumani Masasi, Yohana Msita, Moshi Mmanywa, Adimini Msokwa, Dk Mwanga Mkayagwa, Rashidi Saidi na Francis Shaban.
Manyoni Mashariki: Dk Pius Chaya, Joseph Chitinka, Alex Manonga, Jumanne Mtemi, Daniel Mtuka, Harold Huzi na Gaitani Romwad.
Singida Mashariki: Jonathan Njau, Hamisi Maulid, Mdimi Hongoa, Jocab Kituu, Emmanuel Hume na Martin Lissu.
Ikungi Magharibi: Dinawi Gabaraiel, Hamisi Lissu, Wilson Khambaku, Dk Hamisi Mahuna, Dk Grace Puja, Yona Makala, Elibariki Kingu na Hamisi Ngila.
Iramba Magharibi: Mwigulu Nchemba, David Jairo, Juma Kilimba na Amon Gyuda.
Singida Mjini: Hassan Mazala, Amani Rai, Mussa Sima, Leah Samike, Philemon Kiemi na Juma Kidabu.
Singida Kaskazini: Lazaro Nyalandu, Amosi Makiya, Justin Monko, Michael Mpombo, Sabasaba Manase, Yahana Sinton, Mugwe na Aron Mgogho.
Imeandikwa na Robert Kakwesi, Dinna Maningo, Mussa Juma, Filbert Rweyemamu, Gaspar Andrew na Mussa Juma, Joseph Lyimo, Mussa Mwangoka, Godfrey Kahango na Julius Mathias.
                                    Habari kutoka:http://www.mwananchi.co.tz