Saturday 31 January 2015

NEYMAR NI SHEEDAH LIGI YA HISPANIA.,..CHEKI ALICHOFANYA HAPA

neymar-barcelona-2013-hd-wallpapers-jpg
Kiungo mshambuliaji wa Barcelona Neymar Da Silva Jr vamekuwa kwenye kiwango cha juu msimu huu ambapo amekuwa sehemu muhimu sana ya timu yake katika michezo ya hivi karibuni .

Neymar amedhihirisha ubora wake kwa jinsi ambavyo amekuwa akifunga mabao mfululizo huku akisaidia kwa kutoa pasi za mwisho kwa wenzie na amekuwa akifanya hivyo kwa mwendelezo mzuri ,
Tatizo limekuwa moja tu , jinsi amabvyo mchezaji huyu amekuwa akilaumiwa hasa na wapinzani kwa kuwa mtovu wa nidhamu na mkosefu wa heshima ambapo amekuwa akiwadhihaki wachezaji wa timu pinzani kwenye nyakati tofauti hali ambayo imeonekana kuwakera wengi .
Wapinzani wa Barcelona wamemlalamikia Neymar kwa kitendo chake cha kuwadhihaki anapokuwa uwanjani .
Wapinzani wa Barcelona wamemlalamikia Neymar kwa kitendo chake cha kuwadhihaki anapokuwa uwanjani .
Neymar amekuwa na tabia ya kuwatukana wachezaji wa timu pinzani na wakati mwingine hata kwa vitendo na ndio maana amekuwa kwenye vurugu nyingi ambazo zimekuwa zikitokea kwenye michezo ya Fc Barcelona .
Majuzi wakati wa mchezo war obo fainali ya michuano ya Kombe la Mfalme ambapo Barcelona ilishinda kwa 3-2 Neymar alikuwa kwenye fujo zilizoibuka kati yake na wachezaji wa Atletico ambao ni Gabi , Juan Fran na Raul Garcia.
Ilifikia mpaka kocha Luis Enrique alilazimika kumtoa uwnajani ambapo baadae alikir kufanya hivyo kwa lengo la kumlinda .
Neymar amekuwa akihusika kwneye vurugu zinazotokea uwanjani kutokana na tabia yake ya kuwatukana wachezaji wa timu pinzani .
Neymar amekuwa akihusika kwneye vurugu zinazotokea uwanjani kutokana na tabia yake ya kuwatukana wachezaji wa timu pinzani .
Hivi karibuni Luis Enirque alisikika akisema kuwa Neymar anapaswa kujiheshimu na kuwaheshimu wapinzani na kama asipofanya hivyo huenda akafanywa ‘chambo’ na kuumizwa na wachezaji wa timu pinzani ambao wamejawa na hasira juu yake .
Tabia hii ya Neymar itawakumbusha wengi juu ya kile kilichokuwa kinafanywa na Ronaldinho Gaucho wakati akiwa na klabu hii ya Barcelona ambapo aliripotiwa kuwadhihaki na kuwatusi wapinzani huku akiendelea kuwakera kwa chenga zake za maudhi .
Credit:Millardayo.

TOA MAONI YAKO HAPA

MEYA MANISPAA MOROGORO, WAANDISHI WA HABARI WAPATA AJALI, HABARI KAMILI NA PICHA ZIPO HAPA

Na John Nditi ,Morogoro



MEYA wa Halmashauri ya Manispaa Morogoro , Amir Nondo (45), dereva  na waandishi  wa habari wawili wamepata ajali   baada ya  gari walilokuwa wakisafiria kugongwa na basi la abiria lenye namba za usajili T 831 CEH, aina ya Scania mali ya kampuni ya Happy Africa na kujeruhiwa  sehemu mbalimbali za miili yao na kulazwa  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.



Tukio hilo lilitokea Januari 30, mwaka huu majira ya saa 9: 30 alasiri , eneo la Msamvu Mzambarauni darajani katika barabara kuu ya Morogoro- Dar es Salaam, ambapo basi hilo lilikuwa likotokea mkoani Njombe.



Majina ya watu hao wengine waliojeruhiwa na kulaza katika wodi za daraja la kwanza katika hospitali ya rufaa ya mkoa , ni dereva wa gari la Meya, Mwambala Ally (55) , na waandishi wa habari ambao ni wapigapicha vituo vya televisheni , Anitha Chali (30) pamoja na Hussein Nuha (28).



Mstahiki meya huyo  aliyekuwa kwenye gari ya Halmashauri ya Manispaa hiyo  yenye namba za usajili SM 4151, ikiendeshwa na Mwambala  ambamo pia walikuwemo waandishi wa habari hayo na alikuwa katika msafara wa ziara ya kikazi ya mkuu wa mkoa huo,Dk Rajab Rutengwe.



Meya Nondo akizungumzia  ajali hiyo, akiwa wodini akipatiwa matibabu  ,sambamba na majeruhi wengine alisema baada ya kufika eneo la Mizambarauni, Darajani, lilichomoka pembeni basi la abiria ililokuwa likitokea Njombe kuelekea  Dar es  salaam, na kuligonga kwa mbele gari alilokuwemo.



Mashuhuda wa ajali hiyo  waliwaambia waandishi wa habari wakiwa eneo la tukio,  kuwa  chanzo cha ajali hiyo ni basi la abiria mali ya kampuni ya Happy Africa, kuingilia msafara huo wa mkuu wa mkoa uliokuwa ukielea mjini baada ya kukagua shughuli za ujenzi wa vyumba vya maabara na kuzungumza na wananchi wa Kata ya Bigwa katika  Shule ya Sekondari Sumaye.



Mkuu wa mkoa kwa takribani wiki mbili amekuwa katika ziara katik halmashauri saba za mkoa huo kwa ajili ya kukagua shughuli za ujenzi na umaliziaji wa maabara tatu kwa kila shule ya skondari ya Kata na pia kutumia fursa hiyo kujitambulisha , kusikiliza kero na kuzipatia majawabu ya msingi.



Januari 29 na 30 mwaka huu ilikuwa ni zamu ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Shule ya sekondari Sumaye kilikuwa ni kituo chake cha mwisho katika ziara hiyo na baadaye kufanyika kwa majumuisho ya ziara hiyo Januari 31, mwaka huu mjini Morogoro.



Hata hivyo baada ya kufikishwa hospitali ya rufaa ya mkoa , viongozi mbalimbali walifika kuwajulia hali  wakati wakiendelea kupatia matubabu na madaktari mbingwa wa hospitali hiyo, akiwemo Mganga mkuu wa mkoa , Godfrey Mtei.



Mstahiki Meya Nondo ameumia sehemu ya kichani na mkononi , wakati na mpiga picha Anita Chali, ameumia  kichwani, huku dereva pamoja na  Hussein wakiumia zaidi  kwenye paji la uso na kichwani huku Hussein akisaidiwa na mashine ya kupumulia (oxygen).



 Kufuatia tukio hilo Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa mkoa imesema itatoa taarifa ya ajali hiyo  jumamosi ya  Januari  31, mwaka huu.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Rajab Rutengwe ( wa kwanza kushoto) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Morogoro , Said Amanzi , wakipita eneo ambalo gari la namba SM 4151 Nissan iliyokuwa ikitumiwa na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo , ilipogongwa Januari 30, mwaka huu saa 9: 30 alasiri eneo la Mzambarauni Darajani -Msamvu barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .Meya huyo na watu wengine watatu walijeruhiwa na kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro na kulazwa wakindelea kupatiwa matibabu.
Wasamalia wakimuwahisha Hospital,Mmoja wa majeruhi mara baada ya kupata ajali eneo la Mzambarauni Darajani -Msamvu barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .
Hili ndilo basi lililogongana na Gari ya Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo.
Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo ,(45) akiwa amelazwa wodi namba tano ya daraja la kwanza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya kujeruhiwa kufuatia gari yake SM 4151 ilipogongwa Januari 30, mwaka huu saa 9: 30 alasiri eneo la Mzambarauni Darajani , Msamvu Barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam ,mbali na Meya huyo na watu wengine watatu ,Dereva Mwambala Ally (55), na waandishi wa habari , Anita Chali (30) pamoja na HUSSEIN Nuha (28) pia walijeruhiwa na kulazwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya kupatiwa matibabu. ( Picha na John Nditi).
Mwandishi wa habari,Anita Chali akiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya kujeruhiwa kufuatia gari waliyoipata,walipokuwa kwenye kazi na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo.
Habari na Masamablog

TOA MAONI YAKO HAPA

MGANGA WA DIAMOND PLATNUMZ ATUPWA JELA MIAKA 7 ..KOSA LAKE LIKO HAPA

Stori: Richard Bukos/Amani
Yule mganga aliyejitapa kumtengenezea nyota ya mvuto staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya amehukumiwa kifungo cha miaka saba (7) jela baada ya kukutwa na hatia katika kisa cha kuchanganya akihusishwa na wizi wa gari.
Ustadh Yahya akiwa chini ya ulinzi.
 TUJIUNGE MAHAKAMA YA WILAYA YA ILALA
Habari za uhakika zilieleza kwamba aliyehitimisha kesi hiyo ni Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar, Hassan Kisailo mapema Jumatatu wiki hii wakati jua la asubuhi likiwaka.

 HAKIMU ASHUSHA MIWANI
Huku kijasho chembamba kikimtiririka huku akishusha miwani kidogo kuona wahudhuriaji wa kesi hiyo, Hakimu Kisailo alitoa hukumu hiyo kwa maelezo kwamba, mnamo Januari 20, mwaka jana, maeneo ya Kariakoo jijini Dar, Yahya alidaiwa kuiba gari aina ya Toyota RAV4 lenye namba za usajili T 139 BSJ likiwa na thamani ya Sh. milioni 12, mali ya Edrick Elieza.

 Wakati Hakimu Kisailo akisoma hukumu hiyo, mshtakiwa na wadhamini wake hawakuwepo mahakamani hapo hivyo alisema mara tu baada ya hukumu wahusika hao watakamatwa ili wakatumikie adhabu inayowakabili.
 MAPITIO MTIRIRIKO WA KESI
Huku akiangalia kulia na kushoto, Hakimu Kisailo alisema kuwa, baada ya kuupitia mtiririko wa kesi hiyo, alibaini kwamba ni kweli mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo hivyo alimhukumu kwenda jela miaka 7.

 
...Ustadh Yahya akilaumu yambo.
 BOFYA HAPA KUMSIKIA HAKIMU
Kama ilivyo desturi ya Magazeti ya Global kutaka kujua vitu kwa undani, mwanahabari wetu alizungumza hakimu huyo kuhusiana na hukumu hiyo ambapo alishusha tena miwani kidogo kisha kumwangalia kwa juu na kusema:

 “Ni kweli huyo mnayemuita sijui Mganga wa Diamond nimemhukumu kwenda jela miaka 7, ingawa hakuwepo hapa mahakamani.
“Nasikia alitoroka tangu alipowekewa dhamana lakini kifungo hicho kitaanza muda wowote atakapokamatwa.”

 WADHAMINI NAO WANALO
Hakimu Kisailo alisema kwamba, Ustadh Yahya aliwekewa dhamana na watu wawili, Moses Msangi na Seme Kisusandi ambao wanatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni moja kila mmoja au kwenda jela miezi sita wakati sangoma huyo akisakwa.

 Hakimu Kisailo alisema licha ya jamaa huyo kuingia mitini, wadhamini wake nao hawakuwepo mahakamani hapo na kusema kuwa mkono wa sheria ni mrefu utawafikia popote pale walipo.
 MANENO KUNTU
Mmoja wa mashuhuda wa kike aliyekuwa kwenye chumba cha hakimu huyo alisikika akisema: “Huyo mganga wa Diamond hana lolote, iweje ashindwe kuzima kesi yake na kufikia hatua ya kuhukumiwa kifungo hicho wakati huwa anajidai ni mkali kwenye mambo ya kuwatengenezea watu nyota?
“Unaweza kukuta huko mitaani anajifanya kuwaambia wateja wake ana uwezo wa kuzima ‘makesi’ makubwa-makubwa kumbe hata kesi yake mwenyewe inamshinda.”

 
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
 DIAMOND ATUPIWA LAWAMA
Shuhuda huyo alikwenda mbele zaidi na kumtupia lawama Diamond kwamba alishindwaje kumsaidia mtu aliyempaisha hadi sasa hivi anawiki kimataifa?
 DIAMOND ANASEMAJE
Amani lilimsaka Diamond ili kumfikishia ‘ubuyu’ kuwa mganga wake amehukumiwa miaka sasa jela lakini simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa na hata alipofuatwa nyumbani kwake, Sinza-Mori, Dar, hakuwepo.
 TUMEFIKAJE HAPA?
Ustadh huyo alidaiwa kukamatwa na gari hilo alilodai kufika mikononi mwake kutoka kwa mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mwanahamis. Ustadh alikamatwa  akikatiza nalo Tabora mjini ndipo akawekwa nyuma ya nondo za mahabusu kabla ya kusafirishwa jijini Dar kwa hatua zaidi za kisheria ambazo zimemhukumu kifungo hicho.
Habari na masamablpg.com

TOA MAONI YAKO HAPA

WAFUASI 29 WA CUF WAACHIWA KWA DHAMANA


WAFUASI 29 kati ya 30 waliokuwa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam wameachiwa leo baada ya kutimiza masharti ya dhamana.


Wafuasi hao walikamatwa majuzi huko Mtoni Mtongani, Dar wakati Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba akielekea Mbagala kuwataka wananchi watawanyike baada ya maandamano ya chama hicho kuzuiliwa na jeshi la polisi.



Wafuasi hao 29 wameachiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar baada ya kila mmoja wao kutimiza masharti ya dhamana kwa kutoa kiasi cha shilingi 100,000 pamoja na barua ya mdhamini mmoja ambaye hana hatia.



Mpaka mwandishi wetu anatoka eneo hilo la mahakama, mmoja wa watuhumiwa alikuwa bado mikononi mwa polisi kwa kutokamilisha taratibu za dhamana hiyo akiendelea kumsubiri mdhamini wake aliyechelewesha barua ya udhamini.



Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo amesema kesi yao itatajwa tena Februari 12, 2015
Habari na: masamablog.com

TOA MAONI YAKO HAPA