Wednesday 22 July 2015

ZAIDI YA WAZEE 300 WAMCHANGIA NA KUMCHUKULIA FOMU YA UBUNGE FILIKUNJOMBE JIMBO LA LUDEWA. Wasema wameridhika na utendaji wake.

 Baadhi ya wazee wa wilaya ya Ludewa wakimpa baraka za mwisho za kuanza kugombea kwa awamu ya pili Mh.Deo Filikunjombe
Filikunjombe akisikiliza nasaha za Wazee

 msafara wa kumsikindikiza kutangaza nia ya kugombea ubunge Deo Filikunjombe ukiingia viwanja vya mpira wa miguu Ludewa mjini
Filikunjombe akiwasalimia mamia ya wanachama wa ccm wilayani Ludewa ambao walikuja kumuunga mkono

wasanii wa kikundi cha IVA YOUTH GROUP ambacho ni kikundi cha uhamasishaji wilayani hapa wakifanya yaliyo yao
                                       mamia ya washabiki wa ccm wakimraki Filikunjombe


Filikunjombe akiongea na wananchi wa wilaya ya Ludewa kata ya Ludewa mjini wakati akitangaza nia ya kugombea ubunge

                   msanii wa IVA youth Group Seleman Chikuti akionesha umahiri wake katika sanaa
 Seleman Chikuti toka kundi la IVA youth group linalopatikana Ludewa mjini akifanya vitu vyake wakati Deo Filikunjombe akitangaza rasmi nia ya kugombea ubunge wa jimbo la Ludewa







Zaidi ya Wazee 300 wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wamefanya

maandamano ya kumuunga mkono mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo

Filikunjombe na kumchukulia fomu ya kugombea nafasi ya ubunge wa

jimbo hilo kwa awamu ya pili ili aweze kuliongoza tena kwa kauli ya

kuwa wameridhishwa na utendaji wake ambao hauna mashaka.


Akizungumza kwa niamba ya wazee wenzake mzee Laurent Mtweve alisema

kuwa jimbo la Ludewa limekuwa na umaarufu mkubwa wa kubadili

wabunge kila baada ya miaka mitano kutokana na utendaji

usioridhisha lakini safari hii hakuna haja tena ya kufanya hivyo

kutokana na mafanikio makubwa yaliyofanyika katika kipindi cha

Filikunjombe.


Mzee Mtweve alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2010 HADI 2015

wilaya ya Ludewa imepata mabadiriko makubwa katika kila sekta kwani

wakati mwingine Filikunjombe hakuweza kuisubiri bajeti ya Serikali

alilazimika kutoa fedha za posho yake ili kufanikisha na kutatua

matatizo yanayowakabiri wananchi wake.


Naye Bi.Mariam Nyandoa alisema kuwa katika moja ya kazi ambayo

Filikunjombe anapaswa kuendelea na uongozi ni ile ya kuhakikisha

kila hospitari,zahanati,dispensari kunakuwa na watumishi pamoja na

vitanda vya kujifungulia hali ambayo imekuwa ni kilio cha wanawake

wilayami Ludewa kwa muda mrefu.


Bi.Mariam alisema kuwa kwa sasa hakuna shida tena kama ilivyokuwa

awali kwani unapokwenda hospitari unauhakika wa kupata huduma nzuri

hivyo wazee wote wakaona wachange fedha za kumchukulia fomu ya

kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Ludewa na pia wanaandaa

sherehe ya kumpongeza kwa uongozi wake mzuri ambao ameuonesha.


"Sisi kama wazee katufanyia mengi katika kipindi cha uongozi wake

na yamekuwa ya mafanikio kwa wilaya ya Ludewa kumpata mbunge kijana

na ambaye anatumika akitumwa hivyo tunampango wa kumfanyia sherehe

licha ya kuwa tumemchukulia fomu hivyo hatuna mpango wa kuwa na

mbunge mwingine zaidi yake",alisema Bi.Nyandoa.


Akiongea na umati wa wananchi wa wilaya ya Ludewa katika viwanja

vya michezo Ludewa Mjini wakati akitangaza nia ya kungombea nafasi

ya ubunge Mh.Deo Filikunjombe alisema kuwa mafanikio yote

yaliyopatikana sio juhudi zake binafsi bali ni ushirikiano

alioupata toka kwa wananchi wa jimbo lake.


Filikunjombe alisema kuwa katika kipindi cha uongozi wake ni kweli

kumekuwa na mafanikio makubwa lakini wananchi ndio waliokuwa

wakimsukuma kufanya hayo na wakati mwingine alikuwa mkali Bungeni

kutokana na halia halisi ya ugumu wa maisha ya wananchi wa wilaya

ya Ludewa.


Alisema kuwa anamshukuru rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kwa

kuitendea haki wilaya ya Ludewa kwani katika kipindi cha uongozi wa

ke Ludewa imekuwa ikisikilizwa kupitia yeye hali ambayo

imeharakisha maendeleo wilayani Ludewa.


Anasema katika ubunge wake wa miaka mitano Ludewa imeweza kupata

kipande cha lami na hatimaye barabara za mitaa ya Ludewa mjini

zimeweza kung'ara kwa lami ikiwa ni juhudi zake kwani kabla ya

kuingia katika ubunge wilaya ya Ludewa haikuwa hata na kipande

kimoja cha lami.


Alisema kuwa licha ya Lami lakini barabara za vijijini vimefunguka

mfano barabara ya Lupingu ambapo kwa sasa kuna gari za abiria

zinafika huko wakati awali haikuwezekana pia barabara ya Mawengi

makonde ambako kwa sasa samaki wabichi wa ziwa nyasa wanafika

mapema Ludewa mjini.


Pia katika nishati ya umeme alivikuta vijiji vitatu vta

Mavanga,Mawengi na Ludewa mjini ndivyo vilikuwa na umeme lakini kwa

sasa kunamiradi ya umeme katika vijiji 67 ikiwa wilaya ya Ludewa

inajumla ya vijiji 77 hivyo anatangaza nia ya kugombea tena nafasi

hiyo ili aweze kukamilisha vijiji vilivyobaki.


Filikunjombe alibainisha kuwa wilaya ya Ludewa inatakiwa

kubadirishwa haraka na haya machache ambayo wananchi wanayaona kama

ni mabadiriko makubwa kwake ni machache sana kwani Ludewa imekuwa

nyuma kimaendeleo kwa miaka mingi hivyo katika mipango yake ya

ujenzi wa lami barabara kuu tayari Serikali imeshatoa fedha ya

kujenga barabara hiyo na awamu ya kwanza itajengo kilomita 50.


Alisema ujenzi wa barabara hiyo unaanza mapema mwezi ujao ambapo

Dkt.John Pombe Magufuli atakuja kabla ya kuanza ujenzi ili kujionea

mafanikio aliyoyafanya kwa wananchi wa wilaya ya Ludewa katika

sekta ya miundombinu na baadaye atakuja Rais Dkt.Kikwete kuweka

jiwe la msingi la ujenzi wa viwanda vya chuma cha Liganga na makaa

ya mawe Nchuchuma.


Aliwataka wananchi wa wilaya ya Ludewa kumuunga mkono mgombea wa

nafasi ya urais kupitia chama cha mapinduzi Dkt.Magufuli kwani ni

kiongozi makini na anayeipenda wilaya ya Ludewa kwa ni bila yeye

hata barabara za lami wilayani hapa tusingezipata hivyo wananchi wa

wilaya ya Ludewa wanahaki ya kujivunia kwa kuteuliwa Dkt Magufuli.


Filikunjombe alisema kuwa hivi sasa Serikali imepitisha bajeti ya

ujenzi wa daraja la mto ruhuhu ili kuunganisha wialaya ya Ludewa na

ile ya Nyasa hivyo wananchi wanatakiwa kujiandaa na fulsa ya

kibiashara watakayoweza kufanya na mkoa jirani wa Ruvuma.


Mwisho. 

Habari na: http://habariludewa.blogspot.com

No comments:

Post a Comment