Sunday 29 December 2013

Michezo| TFF yazidi kumhalalisha Ragge kuwa bado ni Mwenyekiti wa Simba.

                 
             Ismail Aden Rage ndiye Mwenyekiti halali wa Simba ambapo Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imemtaka kuitisha Mkutano Mkuu kwa mujibu wa taratibu za klabu ya Simba.Kamati imebaini upungufu kadhaa wa kisheria kwenye uamuzi wa Kamati ya Utendaji ya Simba uliofanywa Novemba 18, 2013 kwa kumsimamisha Mwenyekiti wao. Upungufu huo ni pamoja na ukiukwaji wa Ibara ya 33 ya Katiba ya Simba juu uitishaji wa mkutano, ajenda ya kumsimamisha Mwenyekiti kuwasilishwa kwenye kikao kwa utaratibu wa mengineyo.
          Changamoto nyingi zilizoelekezwa kwa Mwenyekiti huyo zingeweza kupatiwa ufumbuzi kwa kutumia Ibara ya 16(2) ya Katiba ya Simba.Hivyo, agizo za Rais wa TFF, Jamal Malinzi kumtaka Mwenyekiti wa Simba aitishe mkutano lipo palepale. Pia Mwenyekiti ametakiwa kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi ya Makamu Mwenyekiti kwa kuzingatia Katiba ya klabu hiyo.
           Katika mkutano huo wa kujaza nafasi, ndiyo utakaojadili mgogoro kati ya Mwenyekiti na Kamati yake ya Utendaji. Nafasi hiyo kwa sasa inakaimiwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Joseph Itang’are baada ya Geofrey Nyange aliyekuwa akiishikilia kujiuzulu.TFF inakumbusha wanachama wake wote (vyama vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu) kuzingatia Katiba zao. Kamati pia imegundua ukikwaji wa maadili katika suala hili, hivyo, litapelekwa katika kamati husika.
            Kwa vile maslahi ya TFF ni kuona mpira wa miguu unachezwa kwa utulivu, itazikutanisha pande husika wakati wowote kuanzia sasa.Kuhusu mchezaji Emmanuel Okwi ambaye aliuzwa nchini Tunisia, TFF inafahamu kuwa klabu ya Simba bado haijalipwa na itasaidia kufuatilia FIFA fedha za mauzo ya mchezaji huyo.
  
SOURCE: Shaffih Dauda

Tuesday 17 December 2013

Cristiano Ronaldo's message to Sir Alex
Ferguson on #SPOTY awards :
"Hi boss. I have this chance to send you a
message that I want to share with everyone like
you did with me which was unbelievable and I’ll
never forget it in my life.
"When I arrived at Manchester as an 18-year-
old, you were like a father for me in football and
you gave me opportunities and taught me many
things, and I feel glad to send you this message.
"I remember when I was there in the club and I
asked for the No. 28 shirt and you gave me the
No. 7. It put me under a lot of pressure but you
told me it wouldn’t be a problem and that I
would deserve to put this shirt on my body
because I was a fantastic player.
"You taught me how to be a good professional,
a good boy and you deserve this award because
you are a fantastic man and person. You are the
number one.
"Have a good evening and we will keep in touch.
Take care."

Monday 16 December 2013

Sunday 15 December 2013

Barcelona 2-1 Villarreal: Neymar lights up Camp Nou

The Brazilian struck twice to give his side a narrow victory and ensure they remain top of La Liga

Neymar Barcelona Villarreal La Liga 12142013
Getty Images
Neymar struck his fourth and fifth goals inside the space of four days as Barcelona saw off Villarreal 2-1 at Camp Nou on Saturday night.

The Brazilian forward – who scored a hat-trick in Barca's 6-1 thrashing of Celtic in the Champions League on Wednesday – starred again for the Catalan giants, who moved three points clear of second-placed Atletico Madrid with victory.

Neymar got the home side going with a 30th minute penalty, converting successfully after a harsh handball decision against Mario.

Villarreal enjoyed good spells and levelled three minutes after the break thanks to captain Mateo Musacchio's header.

Neymar had the last laugh, though, with the 21-year-old tapping in from close range after excellent build-up work by Cesc Fabregas and Alexis Sanchez with 22 minutes to play.

Despite missing Lionel Messi, Victor Valdes and Dani Alves due to injury, Barcelona still fielded a strong side as head coach Gerardo Martino made five changes with Fabregas and Andres Iniesta among them.

Former Blaugrana forward Giovani dos Santos started against his old club, but Villarreal were without key midfield pair Cani and Bruno, missing through injury and suspension respectively.

Barca started brightly and almost took the lead in the sixth minute as Alex Song fired a half-volley against the inside of the post from close range.

Giovani excited with two smart dribbles, but his runs eventually amounted to nothing, before the hosts took the lead in fortunate circumstances on the half-hour mark.

Mario was adjudged to have handled the ball inside his penalty area after Jordi Alba hit a ball straight at him from only a few yards away.

Referee Ignacio Iglesias pointed to the spot and Neymar calmly slotted past Villarreal goalkeeper Sergio Asenjo and into the bottom-left corner.

Asenjo was at his best six minutes before the break, though, saving well to deny Alexis and keep the margin to one goal at half-time.

And Villarreal levelled three minutes into the second half, as skipper Musacchio lost Marc Bartra and powered in a thumping header from Manuel Trigueros' corner.

Barcelona goalkeeper Jose Manuel Pinto got a hand to the effort but could not keep it out and Giovani shot just wide as the visitors pressed for a second.

The Catalan giants were patient in response and it ultimately paid dividends, as five minutes after Asenjo charged off his line to deny Fabregas, Neymar scored again.

A superb Fabregas ball was chested down by Alexis and instead of shooting – which he could have easily done – the Chilean drew the goalkeeper before squaring for Neymar to net.

Walinda amani 2 wa UN wauwa Mali

 14 Disemba, 2013 - Saa 18:55 GMT
Waasi wa Azawad wamerejea vitani baada ya kutupilia mbali mkataba waliofikia na serikali miezi minne iliyopita
Walinda amani wawili wa Umoja wa Mataifa wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa katika shambulizi la bomu dhidi ya benki inayofanya kazi peke yake mjini Kidal Kaskazini mwa Mali.
Msemaji wa kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini humo, alisema kuwa shambulizi hilo lilifanyika mapema asubuhi kabla ya benki kufunguliwa.
Walinzi hao walikuwa wanalinda benki pekee inayomilikiwa na serikali mjini Kidal ambako waasi wa Tuareg wanataka kujitenga na Mali. Waasi hao walianza uasi wao miaka miwili iliyopita.
Shambulizi hilo linakuja kabla ya duru ya pili ya uchaguzi wabunge.
Hakuna aliyedai kuhusika na shambulizi hilo, lakini kundi la Azawad linalotaka kujitawala Kaskazini mwa Mali limesema kuwa linajiandaa kususia uchaguzi huo.
Mnamo mwezi Novemba, kundi la MNLA lilitupilia mbali mkataba wa Amani uliofikiwa kati yao na serikali miezi minne iliyopita na kuanza tena uasi.

Saturday 30 November 2013

SAMATTA AFUNGA, LAKINI SFAXIEN YAIUA MAZEMBE DAKIKA YA 88 LUBUMBASHI, WAMKOSA MWALI WA CAF HIVI HIVI!

MSHAMBULIAJI Mbwana Ally Samatta na Thomas Emanuel Ulimwengu leo wameshindwa kutimiza ndoto zao za kuwa Watanzania wa kwanza kuvaa Medali za Dhahabu za michuano ya Afrika baada ya klabu yao, Tout Puissant Mazembe kushinda 2-1 dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia, katika fainali ya pili ya Kombe la Shirikisho Uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi, hivyo kuangushwa kwa matokeo ya jumla ya 3-2, baada ya awali kufungwa 2-0 Uwanja Olympique de Rades mjini Tunis katika Fainali ya kwanza.
 




Mazembe ilitakiwa kushinda mabao 3-0 leo nyumbani ili kutwaa taji hilo, na ilionekana kama ingeweza kufanya hivyo baada ya kuongoza kwa mabao 2-0 hadi dakika ya 88, yaliyofungwa na nyota wa Mali, Traore Cheibane dakika ya 10 na Samatta dakika ya 24. Lakini wakati Mazembe wakiwa bize na mashambulizi ya kusaka bao la tatu dakika za lala salama, Ben Youssef akaifungia bao muhimu Sfaxien dakika ya 88 na kuzima ndoto za akina Samatta kuvaa Medali za Dhahabu za Kombe la Shirikisho. Katika mchezo wa kwanza, mabao yaliyoizamisha Mazembe yalifungwa na washambuliaji wa kimataifa wa Gabon, Ibrahim Didier Ndong aliyefunga bao la kwanza dakika ya 16 na mshambuliaji Taha Yassine Khenissi aliyefunga la pili dakika ya 90 na ushei wakimtungua kipa mahiri, Robert Muteba Kidiaba. Washambuliaji wote wa Tanzania, Samatta na Ulimwengu walianza katika kikosi cha Mazembe pamoja na Tressor Mputu Mabi, lakini hawakuweza kuwanusuru mabingwa mara nne Afrika na kipigo hicho. Sfaxien, timu pekee iliyoshinda Kombe la Shirikisho mara mbili tangu kutambulishwa kwa mfumo mpya mwaka 2004, yenye maskani yake katika mji uliozungukwa na bahari ya Mediterranean, Sfax kwa ushindi huo itazawadiwa kitita cha dola za Kimarekani, 625 000, wakati Mazembe watapata dola 432 000.  Sfaxien pia watamenyana na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ya Misri kuwania taji la Super Cup mechi itakayopigwa nchini Misri Februari 2014.  
 
Wachezaji waliokuwa wakiunda kikosi cha Simba SC mwaka 1993 walivalishwa Medali za Fedha pia na Rais mstafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi baada ya kufungwa mabao 2-0 na Stellah Abidjan ya Ivory Coast mwaka 1993 katika fainali ya pili ya Kombe la CAF Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Awali, Simba ilitoa sare ugenini na kuwapa matumaini Watanzania kwamba taji la kwanza kubwa Afrika lingetua nchini mwaka 1993.  Baada ya mchezo huo, Samatta na Ulimwengu watapanda ndege kesho kuelekea Nairobi, Kenya kuungana na kikosi cha Bara, Kilimanjaro Stars kinachoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge.

Monday 25 November 2013

MATATIZO YA SOKA LA BONGO NI HAYA HAPA Mchezaji wa Under 20 wa JKT Ruvu akisaidiwa baada ya kuumia wakati wa michuano ya Uhai Cup, wakati JKT Ruvu ilipocheza na Yanga jana.

Michuano hii ikiwa na Lengo la kuandaa vipaji, Lakini unadhani Lengo litafikiwa kweli hivi?

(Picha: kwa hisani ya BinZubeiry)
Mchezaji wa Under 20 wa JKT Ruvu akisaidiwa baada ya kuumia wakati wa michuano ya Uhai Cup, wakati JKT Ruvu ilipocheza na Yanga jana. Michuano hii ikiwa na Lengo la kuandaa vipaji, Lakini unadhani Lengo litafikiwa kweli hivi? (Picha: kwa hisani ya BinZubeiry)
HUYU NDIO ZITO KABWE KUTOKA KUCHOMEKA BENDERA ZA CHAKA HALAFU LEO UMWAMBIE AONDOKE HANG'OKI MTU HAPA:

Zitto Kabwe akielezea kwa wanahabari kuwa haondoki Chadema kamwe. 

Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema haondoki Chadema ng'o. Adai yeye ni mwanachama halali wa chama hicho, amejiunga na Chadema akiwa na umri wa miaka 16, maisha yake yote ameyatoa kwa ajili ya kukitumikia chama hivyo hawezi kuondoka Chadema.

Ameyasema hayo muda huu wakati akiongea na wanahabari katika chumba cha mkutano kilichopo katika Hoteli ya Serena Posta jijini Dar es Salaam.

 
Dk. Kitila Mkumbo akiwaeleza wanahabari kuwa Zitto Kabwe hausiki na 'Waraka wa Siri'.
Naye Dk. Kitila Mkumbo aliyevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu Chadema amekubali kuwa 'Waraka wa Siri' uliosomwa kwa wanahabari na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu juzi na kusababisha kuwavua vyeo Zitto Kabwe, yeye na Samson Mwigamba ni yeye aliyeuandaa lakini Zitto Kabwe hausiki kabisa.

Wakili wa Zitto Kabwe, Albert Msando ametaja maswali kadhaa ambayo yanahitaji kujibiwa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu yakiwemo:

Wakili wa Zitto Kabwe, Albert Msando akitaja maswali mabayo yanahitaji majibu kutoka kwa Tundu Lissu.
-Utaratibu gani uliotumika kuwavua vyeo akina Zitto Kabwe?

-Ushahidi gani alionao au alioutumia kumvua vyeo Zitto Kabwe na wenzake?

-Sababu gani za kumhusisha Zitto Kabwe katika mkakati wa siri wakati Dk. Kitila amesema hausiki?
-Utaratibu gani utatumika kuwaandalia mashitaka?

Sunday 24 November 2013

Mama wa Zito Kabwe afunguka.

    

"NILIKUWA NAOMBA KILA SIKU ZITTO AFUKUZWE CHADEMA" MAMA ZITTO AFUNGUKA

Dar es Salaam.
Siku moja baada ya Kamati Kuu ya Chadema kumvua uongozi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Taifa wa chama hicho, Zitto Kabwe, mama yake mzazi, Shida Salum ametoa ya moyoni akieleza kuwa kilichomkuta mwanaye kimefunika mabaya mengi yaliyopangwa afanyiwe.


“Kwa upande wangu naona kama ni ushindi kwa Zitto kutokana na jinsi ninavyojua hali ilivyo, mambo yalikuwa ni mengi mno na nikwambie tu, Zitto kuvuliwa uongozi kumefunika hayo yaliyokuwa yamekusudiwa kufanywa dhidi yake. Nilikuwa naomba Mungu  kila siku ili afukuzwe Chadema,” alisema mama huyo wakati akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake Tabata, Dar es Salaam.

Shida Salum alisema kuwa Mungu amemnusuru mwanaye na kusisitiza, “Watu walikaa na kutengeneza ripoti ya siri kuhusu Zitto na kuiweka kwenye mtandao kisha kuituma kwa wanachama wa Chadema wanaowafahamu. Mpaka wanafikia hatua hiyo maana yake ni kwamba wamejaribu njia zote za kummaliza, lakini wameshindwa.”

Alisema kutokana na hali ilivyo hivi sasa amemnyang’anya mwanaye kwa muda simu zake zote za mkononi, kompyuta mpakato (Laptop) pamoja na iPad ili asiwasiliane na watu, kwa maelezo kuwa wapo wenye nia mbaya wanaomsaka kumpa pole za kinafiki. “Kwa sasa nataka mwanangu atulize akili.”
Shida Salum, mbali na kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, pia ni  mwasisi wa  Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (Shivyawata) na Mwenyekiti wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu wa Viungo (Chawata).  


Zitto pamoja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Dk Kitila Mkumbo juzi walivuliwa uongozi kutokana na uamuzi wa kikao cha Kamati Kuu kilichokutana kwa siku mbili, kuanzia Novemba 20 mwaka huu katika Ukumbi wa Blue Pearl jijini Dar es Salaam, wakituhumiwa  kukisaliti chama.  
Mbali ya kuwavua uongozi Zitto, Dk Mkumbo pamoja na  aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Samson Mwigamba, pia Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. 

Kwa uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Jimbo la Kigoma Kaskazini na Uenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC). 

Katika ufafanuzi wake wa jana, Shida aliwataka wanachama wa Chadema kuwa watulivu kwa maelezo kuwa Zitto hajafukuzwa uanachama, “Siku nyingi walikuwa wanamwinda na hata hilo jambo ambalo Chadema wanasema amefanya, hawana uhakika nalo.” 


Juzi wakati akisoma uamuzi wa Kamati Kuu,  mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu alisema wamebaini kuwapo kwa mkakati mkubwa wa watu hao kutimiza malengo hayo ambao umeandikwa katika waraka unaoitwa ‘Mkakati wa Mabadiliko 2013’, ambao umeandaliwa na kikundi kinachojiita ‘Mtandao wa Ushindi’. 

Alisema kikundi hicho vinara wake wapo wanne,  Zitto anajulikana kama Mhusika Mkuu (MM), Mkumbo (M1), Mwigamba (M3) na mtu mwingine wa nne ambaye alieleza kuwa hajatambulika na anatumia jina la M2. 

Mama Zitto ambaye wakati akizungumza na gazeti hili alikuwa amelala kutokana na kusumbuliwa na maradhi alisema, “Kutolewa katika uongozi ni jambo la kawaida.  Zitto hajafukuzwa chama ila anaweza akafukuzwa maana kapewa siku 14 tu za kujieleza.” 

Alisema kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibroad Slaa, kwamba chama hicho walimwondoa Aman Kabourou (aliwahi kuwa Mbunge wa Kigoma Mjini-Chadema)  itakuwa Zitto, inaonyesha jinsi watu walivyo na chuki na mwanaye. 

“Hayo ni maneno ya chuki, maana hata Zitto naye ana watu wake ambao wanaweza kutengeneza aina fulani ya chuki kwa viongozi wa chama na wanaweza kupata wakati mgumu kufanya safari au mikutano yao mikoani,” alisema. 

Alisema tangu siku nyingi ndani ya Chadema kulikuwa na mpango wa kumng’oa Zitto, akifafanua kuwa hata katika kikao cha Kamati Kuu iliibuliwa hoja ya ruzuku za vyama, huku wajumbe wakimshutumu Zitto kwamba kwa nafasi yake na Naibu Katibu Mkuu alitakiwa kuitetea Chadema kuhusu ruzuku.  

Katika vikao vya Kamati ya PAC, Zitto aliingia katika malumbano na chama chake baada ya kutuhumu vyama vya siasa kuwa hesabu zake hazikaguliwi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), huku akitaka ruzuku kwenye vyama hivyo isimamishwe.  

“Zitto alipoingia katika kikao cha Kamati Kuu alishikilia msimamo wake kwamba kama Chadema inachukia ufisadi, nacho lazima kihakikishe kinakaguliwa,” alisema na kuongeza; 

“Wao wanaona ili waweze kusalimika katika suala hili la ruzuku ni lazima wamfukuze Zitto. Chadema hawako sawa, hesabu zao haziko sawa.”  

Alisema kuwa tatizo lililopo ni kuwapo kwa mkakati wa watu fulani kuiyumbisha Chadema , hivyo kila juhudi zinafanywa ili kukitingisha chama hicho kipoteze mwelekeo. 

“Siwezi kusema wamemwonea au hawajamwonea, wao wametumia waraka wa Mwigamba ambao Zitto amekiri katika Kamati Kuu kwamba hajawahi kuusikia wala kuuona, tofauti na Dk Kitila ambaye amesema amewahi kuuona,” alisema na kuongeza; 

“Zitto anahusishwa na kitu ambacho Chadema hawana uhakika nacho, ukiusoma ule waraka katika aya ya mwisho umeandikwa hivi, ‘Huyu mtu tunayefikiria awe mwenyekiti hajaoa,
tumshauri aoe akikataa tutafute mtu mwingine’, maana yake ni kwamba waraka huo ulikuwa haujamfikia Zitto, kama ungekuwa umemfikia Zitto watu hao wasingemwomba Zitto agombee uenyekiti.” Alipoulizwa nafasi yake ndani ya Chadema kutokana na yaliyomkuta mwanaye alisema, “Mimi hawawezi kunitengenezea jambo. Hivi Zitto anaweza kuwa mbaya mimi nikawa mzuri.” 

Mama huyo alieleza kuwa tangu alipovamiwa na majambazi nyumbani kwake, Aprili 19 mwaka huu hajawahi kuhudhuria kikao chochote cha Chadema. “Wale wanaodhani Zitto kaonewa wanatakiwa kuwa wavumilivu na wapole, wasubiri kwani kila kitu kinawezekana.”

Ushauri kwa mwanaye
Alisema kuwa mwanaye ana uamuzi wake na kwamba hata kama Chadema itamfukuza uanachama, haitaweza kumnyang’anya vyeti vyake vya elimu aliyoipata. 

“Zitto anaweza kufanya kazi mahali popote duniani, lakini pia ni mwalimu anaweza kuamua kufundisha. Ubunge ni mgawanyo wa madaraka. Watu wote hatuwezi kuwa wabunge,” alisisitiza.
Alisema wakati Kikao cha Kamati Kuu kikifanyika Zitto alikuwa nje ya nchi na kwamba yeye alimshauri kuhakikisha kuwa anahudhuria kikao hicho. 

“Alipotua tu na ndege aliniambia kuwa kuna foleni na alitaka kukodi pikipiki ili awahi kikao, aliniambia lazima aende ili kujua hatima yake.  

Aliacha gari lake na kwenda na hata mimi nilimsisitizia kwamba ni lazima aende katika kikao,” alisema. Alisema kuwa Zitto alipofika katika kikao hicho aliweza kuzima hoja zote zilizomhusu ikiwamo ya ruzuku za vyama, kwamba baadhi ya wajumbe walipoona amebadili mwelekeo wa kikao, mjumbe mmoja (akamtaja kwa jina) aliibua waraka uliomng’oa Zitto katika wadhifa wake. 

“Unajua Kamati Kuu ilijadili zaidi kuhusu ruzuku. Hata ule waraka uliongezwa maneno baada ya baadhi ya wanachama kumpora Mwigamba laptop yake alipokuwa mkoani Arusha katika kikao cha Chadema,” alisema. 

Huku akiwataja wanachama wa Chadema walioongeza maneno katika waraka huo (wakiwamo wabunge wawili) na viongozi wa ngazi za juu wa Chadema, mama Zitto alisema kilichomkuta mwanaye ni ushindi mkubwa, kwamba alipangiwa kufanyiwa makubwa zaidi ya yaliyomkuta. 

“Hakuna amani maana ukisikia kengele inagongwa hapa nyumbani unasema hao ndiyo wamekuja kumuua Zitto nini, hivi sasa mpaka walinzi wanaolinda hapa wakisikia unakuja nyumbani kwa Zitto lazima wakuandike jina na kukufuatilia,” alisema mama huyo. 

-Mwananchi

 


Wana masumbwi mpo?
Manny “Pac-man” Pacquiao is back on top after battering Brandon "Bam Bam" Rios to take the WBO International Welterweight title in Macau. http://cnn.it/19SAGgU
Moto mbaya ilitokea juzi K.koo hapo dogo akitolewa ndani ya nyumba yao iliyokuwa inaungua moto alikimbizwa hospital mida asubuhi madaktari walisema moto umeingia asilimia 92% usiku wa juzi akafariki tulimpenda Mungu alimpenda zaidi na alizikwa jana saa kumi jioni katika makaburi ya kisutu R.I.P mdogo wetu.