Monday 2 February 2015

BREAKING NEWS..!! BONDIA FRANCIS CHEKA AHUKUMIWA JELA MIAKA 3 KWA KUMPIGA NGUMI MTU

Taarifa iliyoifikia Malunde1 blog hivi punde,inaenleza kuwa Bondia maarufu hapa nchini,Francis Cheka amehukumiwa kifungo cha Miaka mitatu (3) jela kwa kukutwa na hatia ya kumpiga na kumjeruhi Meneja wa Bar yake iliyopo mjini Morogoro.


Cheka alifikishwa kizimbani leo na kusomewa mashtaka ya kushambulia na kuzuru mwili,akidaiwa mnamo julai 02 mwaka 2014, bila uhalali na akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria, alimpiga kwa ngumi maeneo ya kichwani na tumboni, Bahati Kabanda maarufu kama Masika, na kumsababishia maumivu makali.

Hukumu hiyo imetolewa leo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi,Mkoani Morogoro.


Taarifa kamili itawajia baadae kidogo.

TOA MAONI YAKO HAPA