Tuesday 28 July 2015

BASI LAGONGA TRENI YA MIZIGO NA KUUA WANNE - TABORA MJINI




Askari Polisi wakifanya ukaguzi kwa maiti zilizokutwa eneo la ajali hiyo

Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Juma Bwire akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio la ajali mbaya iliyotokea eneo la kata ya Malolo manispaa ya Tabora ambapo watu wanne walikuwa wamepanda basi hilo la kampuni ya Dont Worry ambapo lilisababisha ajali hiyo baada ya kugonga treni ya mizigo,watu kadhaa wamejeruhiwa vibaya na kulazwa hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete.
Eneo la chini la basi hilo la kampuni ya Dont Worry ambalo lilisababisha ajali hiyo ambapo mbali na uzembe wa dereva lakini basi hilo lililokuwa likifanya safari zake kutoka Tabora mjini kwenda Ufuluma wilaya ya Uyui limeonekana sehemu hiyo ya chini imefungwa kamba za mipira kuzuia vyuma vinavyunganishwa na usukani visichomoke kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa maisha ya wasafiri.

No comments:

Post a Comment