Tuesday 28 July 2015

Lowassa na mkewe wakabidhiwa kadi rasmi za chama cha chadema


Waziri mkuu mstaafu Mh: Lowasa leo amekabidhiwa kadi ya uanachama wa chama cha chadema katika hoteli ya bahari beach, kadi hizo zimetolewa kwa lowasa pamoja na mkewe, na mheshimiwa lowasa amesema yeye hana mpango wa kulipa kisasi kama watu wengine wanavyohisi badala yake amesema kama kunamtu anahisi kwamba anamakosa na anaogopa lowasa atalipa kisasi asiogope na badala yake aende mbele za Mungu na kuomba asamehewe. Viongozi wote wa UKAWA wamelizia kunpokea Lowasa.

Rich Mond:
Kwa suala la RICHMOND amesema kwa mtu yeyote mwenye ushahidi na tuhuma hizo ampeleke mahakamani na aache kupiga kelele.

SALAMU:
Dr Makaidi: Anaanza kwa kutoa Salamu kwa , MBowe, Lipumba, Mbatia na Lowasa ambazo zimetoka chama cha chake Cha NLD, na kutaka LOwasa asahau mambo ya CCM na kufuata ya UKAWA.

Makamu / mwenyekiti CUF, Anaanza kwa kutoa Salamu kwa , MBowe, Makaidi, Mbatia na Lowasa na kusema amepigwa na butwaa na kusema ukawa wamepata jembe.
 NCCR MAGEUZI: Anaanza kwa kutoa Salamu kwa , MBowe, Lipumba, Makaidi na Lowasa na kusema wataendelea kulinda hazi za Mh: Lowasa za kuwa waziri mkuu mstaafu na kusema CCM haina haki miliki ya kuimiliki TANZANIA.
 CHADEMA: MBOWE:  Anaanza kwa kutoa Salamu kwa watu wote na kwa, Lipumba, Mbatia na Lowasa, Kwaniaba ya chadema anamkaribisha LOWASA na Familia na watanzania katika Familia ya CHADEMA, Anasema ujio wa Lowasa umezua hofu CCM, anasema alipigiwa simu na watu wa CCM nakuambiwa akimkaribisha Lowasa atakiharibu chama, na anaanza kuwatoa hofu wanachadema kwa kusema hasemi Lowasa ni mtakatifu bali pia chadema sio mahakama ya kuhukumu mtu bila ya ushaidi.

                                     Habari na www.hatasisitupo.blogspot.com

No comments:

Post a Comment