Wednesday 1 July 2015

MIILI YA WATU 144 YAPATIKANA NCHINI INDONESIA KUFUATIA AJALI YA NDEGE

Maafisa wa Indonesia wamesema miili ya watu 144 imepatikana, baada ya ndege ya usafirishaji mizigo ya jeshi kuanguka katika makazi ya watu katika eneo la Medan, hapo jana.

Jeshi limesema hakuna hata mtu mmoja kati ya 122 waliokuwemo kwenye ndege hiyo aina ya Hercules C-130 aliyenusurika kifo baada ya kuanguka na kugonga nyumba pamoja na hoteli na kisha kulipuka moto.

Wengi wa waliokufa inaaminika kuwa ni ndugu na jamaa wa wanajeshi wa Indonesia. Taarifa za hivi karibuni zimesema watu 19 waliokuwa kwenye nyumba wamekufa.
Habari na: http://rweyunga.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment