Friday 5 June 2015

 Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe akipokelewa na wananchi wa kata ya Ibumi kwa shangwe kubwa baada ya kufanya makubwa ya kimaendeleo wilayani Ludewa
                                               hawa ni baadhi ya wananchi waliokuja kumshangilia
                        Barabaea za Mitaa ya Ludewa mjini zikiwa zimejengwa kwa kiwango cha Lami


     Filikunjombe hupokelewa na mabango ya namna hii anapotembelea jimbo la Ludewa na vijiji vyake



                 hizi ni picha za ujenzi wa barabra za lami katika mji wa Ludewa unaoendelea hivi sasa
Wananchi wa wilaya ya Ludewa wamekiri misemo ya vijana wa wilaya hiyo ya Ludewa tuitakayo kutokana na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe kufanikisha kuubadirisha mji wa Ludewa kwa kipindi cha mika mitano ya uongozi wake kama mbunge

wilaya ya Ludewa ni moja ya wilaya zilizosahaulika kwa kipindi cha miaka mingi lakini kupitia Filikunjombe wilaya hiyo imekuwa na maendeleo ya haraka tofauti na miaka mingine  kwani mtu yeyote aliyewahi kuishi katika wilaya hiyo miaka mitano iliyopita akifika sasa ataona mabadiriko makubwa yaliyojitokeza kwa muda mchache.

Hata hivyo Filikunjombe amekuwa akipokewa na mabango yenye jumbe balimbali zinazoonesha kumuunga mkono katika juhudi zake za kimaendeleo zikiambatana na kumchangia fedha kwaajili ya kuchukulia fomu ya kugombea ubunge kwa awamu nyingine tena.
                                                        Habari na Habari Ludewa Blog:

No comments:

Post a Comment