Tuesday 30 June 2015

Wasichana wa Chibok washinikizwa kuua

Wasichana wa Chibok washinikizwa kuua

     Wasichana wa Chibok waliotekwa kaskazini mwa Nigeria zaidi ya mwaka mmoja
Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC limeelezwa kuwa baadhi ya wasichana waliotekwa na wanamgambo mjini Chibok Nigeria wamekuwa wakishinikizwa kuwaua Wakristo.
Wanawake watatu ambao wanasema walikuwa wakishikiliwa katika kambi moja na wasichana hao wanasema wapiganaji wa BOKO HARAM waliwafunga mikono wanaume wa Kikristo. Wasichana hao waliwachinja wanaume hao kwa kuwakata shingo.
Wanawake hao wanasema baadhi ya wasichana hao wa Chibok walikuwa na silaha. Baadhi ya wasichana waliwachapa mateka wengine wa kike. Haikuwa rahisi kuthibitisha ukweli wa taarifa hii. Wasichana 219 kati ya zaidi ya wasichana 270 waliotekwa kutoka shule moja ya bweni ya Chibok bado wanashikiliwa na Boko Haram.
              Habari na: BBC

No comments:

Post a Comment