Monday 8 June 2015

MASKINI:MUONE HUYU PADRE NA WANAFUNZI SITA WALIVYOTETEKETEA KWA MOTO

MASKINI:MUONE HUYU PADRE NA WANAFUNZI SITA WALIVYOTETEKETEA KWA MOTO

WANAFUNZI sita wa Sekondari ya CTC Kigonsera inayomilikiwa na Misheni ya Mbinga mkoani Ruvuma na Mkuu wa Shule hiyo, Padre Yazint Kawonga, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutumbukia bondeni kisha kuwaka moto na kuiteketeza miili yao.


Akizungumza na Mpekuzi juzi shuhuda wa ajali hiyo, Makarius Nchimbi, alisema ilitokea juzi saa tisa alasiri katika mlima uliopo karibu na shule hiyo huku likiwa limewabeba wanafunzi waliokuwa wakitokea shambani kuvuna mahindi ya shule hiyo.


Nchimbi ambaye ni mfanyakazi wa kitengo cha udereva katika misheni hiyo alidai yeye ndiye aliyekuwa dereva wa gari hilo kabla ya kupokelewa na Padre Kawonga aliyemtaka amsaidie kuliendesha kwa kuwarudisha shuleni wanafunzi waliokuwa shamba lililopo Kijiji cha Mkulumus kilichopo Kigonsera.


Alisema gari hilo aina ya Land Rover 110 Station Wagon lenye namba T 306 AYM  lilipofika katika mlima huo lilimshinda Padre Kawonga wakati akitumia gia namba mbili na kuanza kurudi nyuma huku wanafunzi wengine waliokaa juu walifanikiwa kuruka kabla halijatumbukia na baadhi yao 24 waliumia.


Alisema baada ya gari hilo kutumbukia bondeni wao walijitahidi kuingia kwenda kuvunja milango ili waweze kuwaokoa baadhi yao lakini ilishindikana kutokana na nyaya za umeme wa gari kulipuka na kuliunguza huku miili yao ikiwemo ndani  na kusababisha ishindwe kutambulika.


Alisema kutokana na moto kuwaka iliwalazimu watafute mbinu za kuuzima na walitumia maji lakini haikuwezekana na walifanya jitihada ya kuipata winchi iliyoweza kwenda kuliinua gari hilo likiwa limeteketea.


Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Kigonsera, Dk. Patrik Mhagama, alisema kituo hicho kilipokea maiti saba na majeruhi wakiwa 24 na kati ya hao wawili wamepekwa Hospitali ya Mbinga kutokana na hali zao kuwa mbaya huku 17 walitibiwa na kuruhusiwa na watano bado wapo kituoni hapo.


Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikihela, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na alisema taratibu za kuyapata majina halisi ya marehemu bado zinaendelea na zikikamilika zitatolewa taarifa.


Aliwataja majeruhi hao kuwa ni Japheth Komba (16), Regobert Mahai (16), Edgar Maseko (16), Luiza Mbunda, Afa Kifaru (15), Nelalfred Nchimbi (16), Teodora Wolfa (16).
Habari na Masama blog

No comments:

Post a Comment