Tuesday, 7 July 2015

Polisi: Msiokuwa na shughuli maalumu msije Dodoma

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma ,David Misime. 
Na Rachel Chibwete
Kwa ufupi
Misime alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu wiki hii ambayo inatarajiwa kuwa na ugeni mkubwa wa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM ambao amesema kuwa unakadiriwa kuwakusanya watu takribani 10,000.



Dodoma. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime amewataka wageni wasiokuwa na shughuli muhimu ya kufanya mkoani hapa kutokuja katika kipindi cha juma hili ili kuepusha usumbufu utakaojitokeza.
Misime alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu wiki hii ambayo inatarajiwa kuwa na ugeni mkubwa wa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM ambao amesema kuwa unakadiriwa kuwakusanya watu takribani 10,000.
Alisema ili kuepusha usumbufu utakaojitokeza kama vile kukosa mahali pa kulala, ni vyema kama mtu hana shughuli ya muhimu ya kufanya mjini hapa asije mpaka mkutano huo utakapokwisha.
“Kuna wengine wanataka kuja kwa ajili ya ushabiki tu au kuja kushuhudia tukio zima na hata kama hawatakuja haitawaathiri kitu hivyo ni vyema wasije ili kuepusha usumbufu,” alisema Misime.
Alisema Jeshi la Polisi limejipanga kuimarisha ulinzi na usalama kwa wananchi wote watakaofika katika mkutano huo na kuwataka wananchi kutoa taarifa za viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika maeneo yao.
Aliwataka wamiliki wa nyumba za kulala wageni kuhakikisha kuwa vitu vyote vyenye thamani vya wateja wao vinatunzwa vizuri ili kuepusha usumbufu au kupotea kwenye mikono yao.
Ulinzi mkali bungeni
Jana, Polisi waliimarisha ulinzi bungeni kwa kuongeza idadi ya askari na pia kufunga kipande cha barabara kuanzia kwenye mzunguko wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani kupitia eneo la Bunge hadi mwanzo wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Tawi la Dodoma.
Kulikuwa na idadi kubwa ya polisi wa usalama barabarani, utepe mweupe uliofungwa katika barabara hiyo huku kukiwekwa kibao kilichoandikwa kwa maandishi mekundu, “barabara hii imefungwa.”
Alipoulizwa kuhusu hatua hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime (pichani) alisema kufungwa kwa barabara hiyo ni miongoni mwa shughuli za usalama.
                                    Habari na: http://www.mwananchi.co.tz

MAHAKAMA YAWAHUKUMU MRAMBA NA YONA KIFUNGO CHA MIAKA MITATU JELA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana imewahukumu kifungo cha miaka mitatu jela na kulipa faini ya shilingi milioni 5 kila mmoja aliyekuwa Waziri wa Fedha Basil Mramba na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Daniel Yona baada ya kuwatia hatiani kwa makosa mawili.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji John Utamwa, Jaji Sam Rumwenyi pamoja na Hakimu Saul Kinemela ambapo mtuhumiwa wa tatu wa kesi hiyo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja amekutwa hana hatia.

Washitakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na mashitaka ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7 kutokana na kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni ya kukagua madini ya dhahabu ya MS Alex Stewart ya Uingereza.
                                      Habari na: http://rweyunga.blogspot.com

Saturday, 4 July 2015

Majambazi yachakaza gari la polisi kwa risasi

 
Kwa ufupi
Majambazi hayo pamoja na askari polisi waligeuza mtaa huo kuwa eneo la mapambano baada ya kutupiana risasi kwa zaidi ya dakika 15, huku jambazi moja likiuawa kwa kupigwa risasi na askari waliokuwa kwenye mpambano huo.
SHARE THIS STORY
0
Share


Mwanza. Ilikuwa kama sinema, lakini ndivyo ilivyokuwa, majambazi yamelichakaza gari la polisi kwa risasi wakati wakijiandaa kufanya uhalifu eneo la Nyegezi mkoani Mwanza.
Tukio hilo ambalo lilikuwa la aina yake lilitokea kwenye Kata ya Nyegezi, Mtaa wa Igubinya Wilaya ya Nyamagana mkoani hapa.
Majambazi hayo pamoja na askari polisi waligeuza mtaa huo kuwa eneo la mapambano baada ya kutupiana risasi kwa zaidi ya dakika 15, huku jambazi moja likiuawa kwa kupigwa risasi na askari waliokuwa kwenye mpambano huo.
Tukio hilo lilitokea jana saa sita mchana karibu na Kambi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), iliyopo Nyegezi Kona.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema majambazi hao walianza kuonekana saa 3:00 asubuhi, wakipita kwenye eneo hilo kila wakati na kuanza kuwatilia shaka.
Tukio hilo lilizua taharuki baada ya milio ya risasi kuanza kusikika, hali iliyosababisha wapita njia na wafanyabishara kuhaha na kukimbia huku na kule bila kujua kitu gani kimetokea.
Kati ya majambazi hayo alikuwemo mwanamke, ambaye naye alionekana akitupiana risasi na polisi kabla ya kukimbia kwa kutumia usafiri wa pikipiki, baada ya kuzidiwa nguvu na askari hao.
Wanajeshi pia walionekana kufurika kwenye eneo hilo, ambao nao walikuwa wanashuhudia kinachoendelea. Baada ya kuzidiwa nguvu majambazi mawili yalikimbia pembezoni mwa eneo la kambi ya jeshi, jambo lililoelezwa kuwa walikuwa wageni.
Mmoja wa shuhuda wa tukio hilo, Emmanuel John alisema; “Watu hawa walianza kuonekana tangu asubuhi, tuliwatilia shaka, hatukujua wanataka kuiba wapi, lakini baada ya kujua tumewagundua na kwakuwa polisi walikuwa karibu, walikuja ghafla tukaanza kusikia milio ya risasi hewani.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Charles Mkumbo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa watu hao ambao walikuwa watatu walifanikiwa kukimbia baada ya kutupiana risasi na polisi, huku mmoja wao akiuawa baada ya kupigwa risasi ya paja.
Alisema polisi waliliua jambazi moja ambalo walilikuta na silaha aina ya SMG ikiwa risasi 19 ambazo hazijatumika pamoja na maganda ya rasasi 23 zilizotumika katika mapambano hayo.
“Nikweli kumetokea tukio la majambazi ambayo yalikuwa yanazunguka zunguka eneo la Nyegezi kona Mtaa wa Igubinya, walitiliwa shaka na watu wa kawaida baada ya kuwahoji,” alisema Mkumbo na kuongeza:
“Kwa bahati nzuri polisi tayari walikuwa wameweka mtego na walikuwa wamefika kwenye eneo hilo na kuyafuatilia. Majambazi hayo yalianza kupiga risasi, jambo ambalo polisi walikabiliana nalo na kuweza kuwadhibiti.”
Alisema jambazi mmoja aliuawa baada ya kupigwa risasi na wengine watatu wakakimbia, polisi inaendele kuwatafuta ili kuhakikisha wanakamatwa.
Mkumbo alisema gari lao aina Land Rover Defender liliharibiwa baada ya kushambuliwa kwa risasi, lakini hakuna askari aliyejeruhiwa kutokana na tukio hilo.
Eneo la Nyegezi limekuwa na matukio kadhaa ya uharifu ,ambapo mwaka jana matukio mawili yalitokea katika eneo hilo.
                                     Habari na: http://www.mwananchi.co.tz

Friday, 3 July 2015

Wanne wahukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kumuua albino

                 https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcRwp1dXuojJxQfkcrHy6jHhwoxsuGfHSoEp1EDfA_RoIXSleGQA6g

Na Lauden Mwambona, Mwananchi

Mbeya. Washtakiwa wanne kati ya watano wa kesi ya kumuua mtu mwenye ulemavu wa ngozi (albino) Henry Mwakajila mwaka 2008 wilayani Rungwe, wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa mjini hapa jana.
Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Nyanda za Juu Kusini aliwataja waliohukumiwa kuwa ni Hakimu Mwakalinga na Leonard Mwakisole wote wakazi wa Kijiji cha Kiwira wilayani Rungwe na Gerard Kalonge na Asangalwisye Kayuni wa Kijiji cha Mbembati wilayani Ileje.
Mshtakiwa aliyenusurika kwenye kesi hiyo ni Mawazo Figomole ambaye alikuwa mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo ambaye aliachiwa huru baada ya ushahidi kutojitosheleza dhidi yake.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda hiyo, Dk Mary Revila alisema mahakama imeridhika pasipo shaka na ushahidi ulitolewa dhidi ya washtakiwa hao na kwamba, wanastahili kunyongwa hadi kufa huku akisisitiza kwamba ushahidi kwa mshtakiwa namba nne haukujitosheleza.
Awali, ilielezwa mahakamani hapo kwamba Februari 5, mwaka 2008, washtakiwa hao walimteka marehemu Henry akiwa katika Shule ya Sekondari Ukukwe wilayani Rungwe na kwenda kumuua.
Ilielezwa kwamba Mshtakiwa Kayuni ambaye ni mganga wa jadi maarufu kwa jina la Katiti alikutwa na utumbo uliodaiwa kuwa wa binadamu na hatimaye Mkemia Mkuu wa Serikali alithibitisha kwamba ulikuwa wa marehemu Henry.
Ilifafanuliwa kwamba mshtakiwa Kalonge alikutwa na vidole vinne na mifupa 10 iliyodaiwa kuwa ya binadamu na baadaye Mkemia Mkuu wa Serikali kuthibitisha kuwa ilikuwa ya marehemu Henry.
                                                             Habari na: http://www.mwananchi.co.tz

Thursday, 2 July 2015

WAKULIMA KIJIJI CHA AMANI WILAYANI LUDEWA WAFUNDWA ILI KUENDELEA KUZALISHA MAHINDI KWA WINGI.

                                            Siku ya wakulima wa Amani ndivyo ilivyokuwa 
Mgeni rasmi wa hafla hiyo ambaye ni ofisa kilimo wa wilaya ya Ludewa  Bw.Naftari Mundo akiongea na wakulima wa kata ya Mundindi katika kijiji cha Amani

Mkulima wa kijiji cha Amani wilayani Ludewa akitoa maelekezo namna ya elimu aliyoipata na na alivyoweza kuitumia katika uzalishaji wa zao la mahindi


                                        Afisa miradi wa shirika la ACTN Bw.Deogratias Ngotio
                                                                 wakulima wakipata somo

                                   mtaalamu wa mbegu za mahindi Bw.Mbele akiongea na wakulima
                             Mtaalamu wa mbolea toka YARA Bw.Shine akitoa elimu kwa wakulima








Wakulima wa kijiji cha amani wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wamepata elimu ya kilimo bora cha mazao ya mahindi,maharage na soya kupitia mashamba darasa ili kuweza kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao hayo kutokana na kijiji hicho kuwa kinara wa uzalishaji wa mazao ya aina hiyo wilayani hapa na mkoa wa Njombe kwa ujumla.

Elimu hiyo imetolewa hivi karibuni na wafadhiri ambao ni African conservation tillage network(ACTN BRITEN,RUDI na CRDB BANK wakiwa na kauli mbiu isemayo “kilimo hifadhi kwa mazao bora mavuno zaidi gharama nafuu na ardhi yenye rutuba”ikiwa na lengo kuu la kukuza uchumi kwa wakulima ambao wataanza kufanya kazi za kilimo kwa kisasa zaidi.

Akiongea katika hafla ya kufunga mafunzo hayo na wakulima wa kata ya Mundindi katika kijiji cha Amani wilayani Ludewa afisa miradi wa ACTN Bw.Deogratias Ngotio alisema kuwa  muungano wao ni kutoa mafunzo ya miradi shirikishi ya kuongeza tija ya uzalishaji katika nyanda za juu kusini mwa Tanzania kwa mazao ya mahindi,mpunga,maharage na soya kupitia elimu hiyo wakulima wataweza kunafaika na kilimo.

Bw.Ngotio alisema kuwa kilimo kimekuwa ni mzigo kwa wakulima kutokana na wakulima kutokuwa na elimu ya kutosha ya kilimo hivyo wadau wa kilimo nchini wameona ni bora kutoa elimu ya kilimo bora na kuhifadhi ardhi yenye rutuba ili kilimo kiweze kuwa ni ukombozi kwa wakulima na sio mzigo wa wakulima kama inavyoonesha katika meneo mengi.
 

Alisema kuwa wakulima walio wengi wamekuwa wakilima maeneo makubwa na kupata mavuno kidogo hali inayowakatisha tama wakulima na wengine huachana na kilimo kwa kuona hakina faida ikiwa haya yate husababishwa na elimu duni waliyonayo wakulima wa Nyanda za juu kusini lakini kwa kupitia wadau mbalimbali wa kilimo wanaoweza kutoa elimu baadhi ya wakulima wameshaanda kutambua umuhimu wa kilimo katika uchumi wa taifa na maisha yao kwa ujumla.

“tumegundua kuwa baadhi ya wakulima wanakatishwa tama ya kuendelea na kilimo kutokana na ukosefu wa elimu ya kutosha kuhusiana na kilimo bora lakini kutokana na muungano wetu kwa pamoja tumeweza kutoa elimu ya shamba darasa ambapo baadhi ya wakulima wameanza kupata mafanikio kupitia mafunzo yetu hali ambayo inatupatia moyo wa kuendelea na mafunzo haya maeneo mbalimbali ili kuweza kuwainua wakulima katika mavuno zaidi”,alisema Bw.Ngotio.

Mmoja wa wakulima  wa Kijiji cha Amani Bw.Fransis Mlelwa alisema kuwa  kijiji hicho kinachoongoza wilayani Ludewa na mkoa wa Njombe kwa uzalishaji wa mazao ya mahindi na maharage ambapo mkulima wa hali ya chini anauwezo wa kuvuna magunia 1500 katika msimu mmoja wa kilimo kwa hali hiyo mashirika mbalimbali yameweza kuungana kuanza kutoa elimu ya kilimo bora.

Bw.Mlelwa alisema kuwa licha ya kupata mafunzo hayo ambayo ni msaada mkubwa kwao katika uzalishaji pia changamoto kubwa inayowakabili wakulima wa kijiji hicho ni upatikanaji wa masoko ya mahindi wakati wa mavuno kwani kumekuwana na shida kubwa kutokana na uzalishaji mkubwa wa mahindi walio nao.

Alisema licha ya kuwa Serikali imekuwa ikiyanunua mahindi kupitia wakala wa hifadhi ya chakula ya Taifa lakini bado wakulima wamekuwa wakibaki na kiasi kikubwa cha mahindi na kushindwa kupata masoko hivyo aliiomba Serikali kuiangalia upya wilaya ya Ludewa kutokana na uzalishaji mkubwa wa zao la mahindi unaofanyika.

Mgeni rasmi wa hafla hiyo ya mafunzo ya shamba darasa ambaye ni ofisa kilimo wa wilaya ya Ludewa Bw.Naftari Mundo akitoa hotuba yake kwa wakulima hao alisema kuwa anatoa pongezi kwa shirika la ACTN kwa kubuni mafunzo hayo ambayo yatainua uchumi wa wakulima na Taifa kwa ujumla katika mpango mzima wa uboreshaji wa kilimo nchini.

Bw.Mundo alisema kuwa Serikali bado inaangalia uwezekano wa kutafuta mashirika mbalimbali ya nje ya nchi ili yaweze kuyanunua mazao ya wakulima kwa bei nzuri hivyo wakulima hawapaswi kukata tama ya kuendelea na kilimo kutokana na kukosa masoko kwani tayari juhudi za ununuzi wa mazao yao zimeshafanyika.

Aidha aliwataka wadau mbalimbali wa kilimo kuiga mfano wa ACTN na washirika wake katika kuendeleza kilimo nchini ili kuweza kuinua pato la taifa na kutengeneza maisha bora ya wakulima kwani kilimo nio msingi wa maisha ya mtanzania bila kilimo hakuna chakula.

mwisho.
                                              Habari na: http://habariludewa.blogspot.com

Wednesday, 1 July 2015

MIILI YA WATU 144 YAPATIKANA NCHINI INDONESIA KUFUATIA AJALI YA NDEGE

Maafisa wa Indonesia wamesema miili ya watu 144 imepatikana, baada ya ndege ya usafirishaji mizigo ya jeshi kuanguka katika makazi ya watu katika eneo la Medan, hapo jana.

Jeshi limesema hakuna hata mtu mmoja kati ya 122 waliokuwemo kwenye ndege hiyo aina ya Hercules C-130 aliyenusurika kifo baada ya kuanguka na kugonga nyumba pamoja na hoteli na kisha kulipuka moto.

Wengi wa waliokufa inaaminika kuwa ni ndugu na jamaa wa wanajeshi wa Indonesia. Taarifa za hivi karibuni zimesema watu 19 waliokuwa kwenye nyumba wamekufa.
Habari na: http://rweyunga.blogspot.com/

LOWASSA ARUDISHA FOMU LEO MJINI DODOMA, ATEMA CHECHE KWA WANAOMTUHUMU


Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa (katikati) akizipanga vyema fomu zake ili azikabidhi kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Rajab Luhavi (kushoto), wakati alipofika kwenye Ofisi ya CCM Makao Makuu, Mjini Dodoma leo Julai 1, 2015. Mh. Lowassa amerudisha fomu hizo, baada ya ziara yake ya nchi nzima kutafuta saini za WanaCCM wa kumdhamini ili apate ridhaa ya chama chake kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015, ambapo jumla ya WanaCCM 874,297 walimdhamini.Kushoto kwa Mh. Lowassa ni Mkewe, Mama Regina Lowassa.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa (katikati) akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Rajab Luhavi fomu za wanaCCM waliomdhamini ili aweze kuwania Uteuzi wa CCM wa kugombea urais kwenye kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Kulia ni Mke wa Mh. Lowassa, Mama Regina Lowassa.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Rajab Luhavi wakionyesha fomu hizo kwa wanahabari wakati wakikabidhiana, kwenye Ofisi ya CCM Makao Makuu, Mjini Dodoma leo Julai 1, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kurudisha fomu za wanaCCM waliomdhamini ili apare baada ya ziara yake ya nchi nzima kutafuta saini za WanaCCM wa kumdhamini ili aweze kuwania Uteuzi wa CCM wa kugombea urais kwenye kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.

               Sehemu ya Viongozi mbalimbali wa CCM waliomsindikiza Mh. Lowassa.
Mmoja wa Wanasiasa wakongwe nchini, Mzee Pancras Ndejembi akizungumza machache kumuhusu Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa pamoja na uwezo wake kwenye Chama cha Mapinduzi na kutamka kumuunga mkono kwa asilimia 100.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiteta jambo na Mkewe, Mama Regina Lowassa.
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM kutoka Zanzibar, Mzee BoraAfya Ame Silima akitoa neno.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu akisema machache juu ya imani yake kwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida akisema machache juu ya imani yake kwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa.
Mwanasiasa Mkongwe nchini, Mzee Kingunge Ngombale Mwilu akiweka msisitizo wa aliyoyazungumza siku za nyuma kumuhusu Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza jambo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Ndg. Hamis Mngeja na Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM kutoka Zanzibar, Mzee BoraAfya Ame Silima, wakati wakitoka kwenye Ofisi ya CCM Makao Makuu, Mjini Dodoma leo Julai 1, 2015.
Picha ya Pamoja na baadhi ya Wenyeviti wa CCM kutoka Mikoa 12 waliomsindikiza Mh. Lowassa kurudisha fomu za udhamini.
                                                                         Wapigapicha wakitafuta taswira.
Wakongwe wakiongozana: Kulia ni Mzee Kingunge Ngombale Mwilu na Mzee Pancras Ndejembi.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwaaga WanaCCM nje ya Makao Makuu ya Chama, Mjini Dodoma leo Julai 1, 2015.

WAZIRI Mkuu Mstafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa, amerejesha fomu za kuomba kuteuliwa kuwania kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu.

Mh. Lowassa ambaye alikuwa amesindikizwa na Wenyeviti wa CCM wa mikoa 12 kutoka bara na visiwani, aliwasili makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma majira ya saa 8:30 mchana wa leo Julai 1, 2015, na kupokewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania Bara), Rajabu Luhavi.

Baada ya kukabidhi fomu hizo, Mh. Lowassa, alikutana na waandishi wa habari na kusoma taarifa yake fupi, ambapo alionya wale wote wanaoeneza habari potofu kuwa yeye ni mla rusha, watoe ushahidi, wapi amekula rushwa, na ni kiasi gani, za nani na wapi, Awataka Watanzania kupuuza habari hizo na kwani yeye ni muadilifu na hana shaka na hilo. Alisema, yeye ana fedha kiasi gani za kuwapa Wana CCM 874,297, waliojitokeza kumdhamini.

"Maneno hayo sasa basi, natoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi huo autoe hadharani vinginevyo waache kueneza uvumi na uongo" Alisema Mh. Lowassa. Alisema yeye anachukia umasikini, na kwamba endapo chama kitamteua na hatimaye Watanzania kumchagua kuwa Rais wa awamu ya Tano, atahakikisha anatimiza dhamira yake ya kuwaondolea Watanzania umasikini.

Mh. Lowassa, ambaye alisindikizwa na Vigogo wa chama hicho akiwemo, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, na Mzee Pankrans Ndejembi wakiwemo wenyeviti wa CCM 12 kutoka Tanzania Bara na Visiwani, amehitimisha zoezi hilo baada ya kuzunguka mikoa 31 ya Tanzania Bara na Visiwani, na mara zote amekuwa akipata idadi kubwa ya wana CCM na wananchi waliojitokeza kwenye ofisi za CCM mahala alikopita, ikiwa ni pamoja na wengine kujipanga barabarani na kumpungia mikono.
                                Habari na: http://rweyunga.blogspot.com

Tuesday, 30 June 2015

CHADEMA WATIFUANA LUDEWA MZIMU WA UKABILA WAWATAFUNA

 

Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe kimeingia katika mgogoro mkubwa kutokana na wanachama wa chama hicho kushangazwa na kitendo cha uongozi wa chama hicho kutoka kanda ofisi za mkoa wa Mbeya kufanya uchaguzi wa viongozi wa wilaya kwa kushitukiza.

Wakiongea kwa nyakazi tofauti baadhi ya wananchama wa chama hicho hapa wilayani kwa masharti ya kutotajwa majina yao kwa kuhofia kuvuliwa uanachama walisema kuwa licha ya kuwa uongozi wa awali ulikuwa na mapungufu ya kuwa na migogoro ya mara kwa mara hasa katika kuendekeza ukabila lakini ulikuwa na watu wenye uwezo wa kufanya maamuzi kutokana na elimu waliokuwa nayo.

Walisema kuwa kitendo cha viongozi wa kanda kuitisha mkutano mkuu wa dharula na kufanya uchaguzi wa viongozi wengine kimewashitua wanachama hao ambao walikuwa na imani kubwa na viongozi wao wa awali hivyo kuwaletea viongozi wengine ni sawa na kukivuruga chama na kusababisha kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu ujao.

Aliyekuwa katibu mwenezi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Ludewa Bw.Kathbet Haule apotakiwa kutolea maelezo kuhusiana na mgogoro huo unaokitafuna chama alisema kuwa viongozi wa wilaya akiwemo yeye kama katibu mwenezi hawajavuliwa madaraka  na nib ado wao ni viongozi wa wilaya licha ya kuwa waliochaguliwa kupitia uongozi wa kanda wanajinadi kuwa wao ndio viongozi.

“sisi ni viongozi wa chadema wilaya ya Ludewa nabado tunatambulika waliochaguliwa ni tume tu kama taxforce itakayofanya kazi katika kipindi hiki cha uchaguzi lakini sisi tutabaki kuwa viongozi wa wilaya na kama wanawatangazia watu kuwa sisi tumepigwa chini huo ni uongo kwani kazi ya ofisi ya kanda si kuchagua viongozi wa wilaya”,alisema Bw.Haule.

Kuhusiana na mgogoro mkubwa unaokitafuna chama hicho wilayani hapa Bw.Haule alisema kuwa ni kweli baadhi ya viongozi ndani ya chama wamekuwa wakishindwa kuelewana kutokana na baadhi ya mambo mfano ni katibu na mwenyekiti ndio walikuwa na mgogoro ambao ungeweza kumalizika kabla ya kufanya uchaguzi uliofanyika. 

Bw.Haule alisema kuwa suala la ukabila ndani ya chama hicho wilayani Ludewa limekuwa likuzungumzwa mara kwa mara licha ya kuwa hakuna malalamiko kwa maandishi yaliyowahi wasilishwa katika ofisi yake na katibu ila kumekuwa na minong’ono kwa baadhi ya wanachama kulalamikia jambo hilo hivyo hakuna uhakika kama jambo hilo ni chanzo cha migogoro ndani ya chama.
                          Habari na: http://habariludewa.blogspot.com

Wasichana wa Chibok washinikizwa kuua

Wasichana wa Chibok washinikizwa kuua

     Wasichana wa Chibok waliotekwa kaskazini mwa Nigeria zaidi ya mwaka mmoja
Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC limeelezwa kuwa baadhi ya wasichana waliotekwa na wanamgambo mjini Chibok Nigeria wamekuwa wakishinikizwa kuwaua Wakristo.
Wanawake watatu ambao wanasema walikuwa wakishikiliwa katika kambi moja na wasichana hao wanasema wapiganaji wa BOKO HARAM waliwafunga mikono wanaume wa Kikristo. Wasichana hao waliwachinja wanaume hao kwa kuwakata shingo.
Wanawake hao wanasema baadhi ya wasichana hao wa Chibok walikuwa na silaha. Baadhi ya wasichana waliwachapa mateka wengine wa kike. Haikuwa rahisi kuthibitisha ukweli wa taarifa hii. Wasichana 219 kati ya zaidi ya wasichana 270 waliotekwa kutoka shule moja ya bweni ya Chibok bado wanashikiliwa na Boko Haram.
              Habari na: BBC

Ghana yazindua gari lake linalojulikana kwa jina la KANTANKA

Ghana yazindua gari lake linalojulikana kwa jina la KANTANKA

Gari la kantanka nchini Ghana
Wakati unapoangazia swala la utengezaji magari mataifa ya Afrika kwa kawaida hayaorodheshwi katika swala hilo.
Lakini hilo sasa huenda likabadilika kufuatia kuwasili kwa kampuni ya magari ya Ghana Kantanka ambayo hivi karibuni yataanza kuingia katika soko.
Miongoni mwa magari ya kampuni hiyo ni lile la lita mbili aina ya 4 by 4 ambalo linatarajiwa kuuzwa kwa takriban pauni 14,000.
null
Gari aina ya kantanka
Lakini je,kampuni hiyo itaweza kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa magari kama vile Toyota,Land Rover na BMW?.
Kwadwo sarfo ni mwana wa mmiliki wa magari hayo.
Babaake ni m'bunifu ambaye pia ni kiongozi wa dini.Hupata fedha kutokana na kilimo na uchimbaji.
Magari ya Kantanka yanafananishwa na magari makubwa kama vile Toyota Prado ama MItsubishi Pajero.
null
Magari aina ya kantanka
Mbele ya gari hilo kuna michoro ya kucha za chui pamoja na nembo ya kampuni hiyo ya nyota ya Afrika.
Kulingana na raia mmoja wa Ghana uvumbuzi kama huo haujafanyika nchini humo.
Tunapenda kununua bidhaa kutoka nje kwa hivyo italazimu kufanyika kwa mauzo ya ziada kwa gari hizi za kantanka kukubalika.
Profesa Robert Ebo Hinson ambaye ni mkuu wa kitengo cha mauzo katika chuo kikuu cha Ghana:Nadhani kile kilichotokea hapo awali ni kwamba tumefanywa tuamini kwamba kile kinachotengezwa katika mataifa ya magharibi ni
null
Gari aina ya kantanka
bora zaidi kwa sababu zote zile.
Wakati mwengine bidhaa zinazotengezwa kutoka Ghana haziwezi kudumu.
Serikali ya Ghana inaelewa kikwazo hicho na tayari imeanzisha kampeni kubwa ya kuwafanya wakaazi kununua bidhaa zinazotengezwa nchini humo.
Waziri wa biashara daktari Ekow Spio Gabrah anaongoza kampeni hiyo na anasema:Nitaendesha moja ya magari haya,kwa kweli niliketia gari moja wakati lilipokuwa likitengezwa na nafurahi kuwa na moja kama gari langu rasmi.
null
Magari aina ya kantanka kutoka Ghana
Waziri na rais wana uwezo wa kuendesha magari hayo kwa gharama ya walipa ushuru.
Lakini je,raia wataweza kutumia fedha zao wenyewe kulipia gharama za kulinunua gari hilo?
Inaonekana kwamba raia wengi kama alivyodai hapo awali Professa wana wasiwasi kuhusu usalama wa gari hilo na kudumu kwake.
null
Gari aina ya kantanka
Je, unadhani wasiwasi huo huenda ukaathiri uzalishaji wa magari hayo? Kulingana na Kwadwo Sarfo gari hilo la kwanza kutengezwa nchini Ghana litapata umaarufu.
                                           Habari na: BBC