Friday, 5 June 2015

 Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe akipokelewa na wananchi wa kata ya Ibumi kwa shangwe kubwa baada ya kufanya makubwa ya kimaendeleo wilayani Ludewa
                                               hawa ni baadhi ya wananchi waliokuja kumshangilia
                        Barabaea za Mitaa ya Ludewa mjini zikiwa zimejengwa kwa kiwango cha Lami


     Filikunjombe hupokelewa na mabango ya namna hii anapotembelea jimbo la Ludewa na vijiji vyake



                 hizi ni picha za ujenzi wa barabra za lami katika mji wa Ludewa unaoendelea hivi sasa
Wananchi wa wilaya ya Ludewa wamekiri misemo ya vijana wa wilaya hiyo ya Ludewa tuitakayo kutokana na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe kufanikisha kuubadirisha mji wa Ludewa kwa kipindi cha mika mitano ya uongozi wake kama mbunge

wilaya ya Ludewa ni moja ya wilaya zilizosahaulika kwa kipindi cha miaka mingi lakini kupitia Filikunjombe wilaya hiyo imekuwa na maendeleo ya haraka tofauti na miaka mingine  kwani mtu yeyote aliyewahi kuishi katika wilaya hiyo miaka mitano iliyopita akifika sasa ataona mabadiriko makubwa yaliyojitokeza kwa muda mchache.

Hata hivyo Filikunjombe amekuwa akipokewa na mabango yenye jumbe balimbali zinazoonesha kumuunga mkono katika juhudi zake za kimaendeleo zikiambatana na kumchangia fedha kwaajili ya kuchukulia fomu ya kugombea ubunge kwa awamu nyingine tena.
                                                        Habari na Habari Ludewa Blog:

LOWASSA: SINA MPANGO WA KUSHINDWA,AFUNGUKA MAZITO..HEBU MSIKIE HAPA

LOWASSA: SINA MPANGO WA KUSHINDWA,AFUNGUKA MAZITO..HEBU MSIKIE HAPA

Lowassa, amechukua rasmi fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku akisema hana mpango wa kushindwa.

Lowassa aliwasili katika Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma jana saa 10:20 jioni akiambatana na mkewe, Regina huku akisindikizwa na wabunge mbalimbali pamoja na wanachama wa CCM.

Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wanachama waliokuwapo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya CCM mara baada ya kuchukua fomu, Lowassa alisema hawezi kuzungumzia upande wa kushindwa katika safari yake.

“Swali rahisi sana, sina mpango wa kushindwa,” alisema Lowassa alipokuwa akijibu swali aliloulizwa na waandishi wa habari kama atashindwa katika kinyang’anyoro hicho.

Alipoulizwa kuhusu hali ya nchi kuwa na watu wanaoshambuliwa, Lowassa alisema atajenga Serikali itakayojali utu na uhuru wa vyombo vya habari.

“Kwanza nimpe pole yule mwandishi aliyeteswa. Sikubaliani na mambo ya kuingilia uhuru wa watu kuteswa. Serikali yangu itaheshimu uhuru wa vyombo vya habari,” alisema Lowassa huku akishangiliwa na wanachama wa CCM waliokuwa wamefurika ndani na nje ya ukumbi huo.

Alipoulizwa kwanini anahusishwa na vitendo vya ufisadi, Lowassa aliyekuwa akijibu maswali kwa ufupi, alisema kama kuna mtu ana ushahidi na tuhuma hizo amtaje jina.

“Kama hawakunitaja hawakunihusisha… Mtu anayejiamini aseme, na anitaje. Nachoka na siasa za tuhuma, hatupimi viongozi kwa rekodi za matusi ila tutawapima kwa matendo yao,” alisema.

Kada huyo wa CCM alivitaka vyombo vya habari kutoshabikia tuhuma zisizo na ushahidi, huku akisisitiza kuwa kila mtu apimwe kwa rekodi yake.

Kuhusu uteuzi wa mawaziri, Lowassa hakutaka kulizungumzia akisema bado hajavuka daraja.
“Nitavuka daraja nitakapolifikia,” alisema.

Kuhusu Serikali ya Umoja wa Kitaifa, alisema ni sera ya CCM iliyotekelezwa baada ya kutokea mgogoro kati ya vyama vya CCM na CUF.

“Angalieni kule Marekani, vyama vya Democrat na Republican, vinashindana kwa kura chache sana. Hata sisi tunapishana kwa kura chache, mimi nadhani kama hatupishani sana hivyo hilo ndilo suluhisho,” alisema.

Awali Lowassa aliwashukuru wana CCM waliofurika katika ukumbi huo akisema anajua kero za chama hicho na atakapokuwa rais atazishughulikia.

“Nawashukuru kwa kunileta nyumbani, nimeitumikia CCM kwa muda mrefu. Nilieleza Dodoma na Arusha nia yangu. Naelewa matatizo wanayopata watumishi wa CCM, nayaelewa. Mishahara midogo, hawakopesheki, hawana fedha za likizo na hawana uchumi mzuri. Wakati wengine wanajengewa nyumba na mikopo wenyewe hawapati,” alisema Lowassa.

Hata hivyo, alimsifu Rais Jakaya Kikwete kwa kuimarisha uchumi ndani ya chama hicho, lakini akasema akiwa rais atafanya zaidi.

“Tunaweza kufanya zaidi, tusiwe ombaomba. Nilipokuwa mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini tumejenga jengo la ghorofa 22 Dar es Salaam. Tuna viwanja na maeneo mengi. Nikichaguliwa kuwa rais na mwenyekiti nitaangalia hilo…Bila CCM madhubuti nchi yetu itayumba,” alisema.

Baada ya mkutano huo, Lowassa alikwenda kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Dodoma kupata udhamini wa chama hicho ambapo Mwenyekiti mstaafu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Pancras Ndejembi alikuwa miongoni mwa wanachama waliomdhamini, akiwamo mlemavu wa miguu, Idd Omari.

Baadhi ya vigogo waliokuwa ukumbini ni pamoja na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga, Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba na Mbunge wa Viti Maalum, Anna Abdallah.

Akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Dodoma Mjini baada ya kuchukua fomu, Lowassa alisema vigelele na makofi anavyopigiwa sasa haviwezi kumpeleka Ikulu isipokuwa wananchi wanapaswa kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura ili iwe njia rahisi ya yeye kuwa mkuu wa nchi.

“Naomba watu wajiandikishe, hakikisheni watoto wenu, wajomba na hata washikaji zetu wanajiandikisha katika Daftari la Wapigakura na nitarudi tena kwenu kuomba kura,” alisema.

Huku akishangiliwa na mamia ya wakazi wa Dodoma, Lowassa aliwaambia amekwenda kuomba wadhamini na si kuomba kura, kwani amebanwa na sheria na utaratibu wa chama chao.

Alisema ameguswa na mapokezi waliyompa na kuwashukuru wadhamini wake kwa kumwamini na kusisitiza kuwa atarudi tena kuomba kura.

“Leo siombi kura, naweka akiba ya maneno hata wakihesabu nina kampeni potelea mbali, lakini nilipokuwa waziri mkuu nilianza kuijenga Ikulu mnayoiona mpaka leo haijakamilika, nitakuja kuikamilisha, maana yake nini, nahamia Ikulu Dodoma,” alisema mbunge huyo wa Monduli huku akishangiliwa na mamia ya wananchi hao.
Habari na Masamablog.

Monday, 25 May 2015

Wimbi la Joto lawaua watu 430 India

Takriban watu 430 wamekufa kutokana na wimbi la joto linalovuma nchini India. 


Takriban watu 430 wamekufa kutokana na wimbi la joto linalovuma nchini India.
Watafiti wamesajili kiwango cha juu mno cha nyuzijoto 48'C katika maeneo mengi nchini humo.
Vifo vingi zaidi vimeripotiwa katika majimbo ya kusini ya Telangana na Andhra Pradesh, ambapo watu 140 wamepoteza maisha yao kuanzia jumamosi wimbi hilo la joto lilipotokea.
Mji wa Allahabad ulioko Uttar Pradesh ulisajili vipimo vya nyuzijoto 48C huku wakaazi wa mji mkuu wa India New Delhi ukistahimili kiwango cha nyuzijoto 44C .


Watafiti wamesajili kiwango cha juu mno cha nyuzijoto 48'C katika maeneo mengi nchini humo.
Maafisa wa utawala nchini humo wameanza kampeini ya kuwahamasisha wanainchi kukaa majumbani mwao na kuwashauri wanye waji mengi.
Yamkini viwango vya joto vimekuwa juu zaidi katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita lakini vifo vimeanza kuripotiwa mwishoni mwa juma.
Jimbo la Andhra Pradesh ndilo lililopoteza watu wengi zaidi ikiwa na jumla ya watu 246 waliopoteza maisha yao kuanzia juma lililopita.


Jimbo la Andhra Pradesh ndilo lililopoteza watu wengi zaidi ikiwa na jumla ya watu 246
"asilimia kubwa ya wale waliopoteza maisha ni watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50 walioshinda nje ya majumba yao.'' alisema kamishna wa kupambana na majanga katika jimbo la Andhra Pradesh.
Wakfu wa waandishi wa habari wanasema kuwa watu 186 wameaga katika wilaya 10 za jimbo la Telangana.
Watu 58 wamekufa kuanzia siku ya jumamosi.
Idara ya utabiri wa hali ya hewa imesema kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa hali hiyo ya joto kuendelea kwa siku kadha zijazo.


Wenyeji wameshauriwa kukaa ndani na kunywa maji mengi
Watu wengine kumi walpoteza maisha yao katika jimbo la Magharibi mwa Bengal.
Waendesha teksi ambazo hazina kiyoyozi hawataruhusiwa kuhudumu kwa saa tano katika mji mkuu wa Kolkata. Hii inafuatia vifo vya madereva wawili.

Idara ya utabiri wa hali ya hewa inasema kuwa hali hiyo ya juu ya joto inatokana na ukosefu wa mvua.

Familia ya mtoto aliyegongwa na fuso na kukatwa miguu anaomba msaada wa kisheria


Naibu Kamanda wa UVCCM ,Innocent Melleck akiwa na mama mzazi wa mtoto Felista ,Beatrice Shirima mara baada ya kukabidhi kiti cha walemavu cha magurudumu kwa ajili ya kusaidia kutoka eneo moja hadi jingine.
Naibu kamanda wa UVCCM wilaya ya Moshi vijijini ,Innocent Melleck akikabidhi Pempers kwa mama wa mtoto Felista ,Beatrice Shirima kwa ajili ya kumsaidia mtoto huyo aliyepata ulemavu wa miguu miwli baada ya kugongwa na gari aina ya Fuso.(Na Dixon Busagaga).
Naibu kamanda wa UVCCM wilaya ya Moshi Vijijini ,Innocent Melleck akiwa amembeba mtoto Felista Shirima(3) aliyekatwa miguu yote miwili baada ya kugongwa na gari aina ya Fuso jirani na nyubani kwao.

Akizungumzia sakata la mtoto huyo Naibu kamanda huyo alisema kuwa ataumia kila aina ya uwezo na nguvu zake kwa kushirikiana na ofisi ya umoja wa vijana wa chama chama mapinduzi UVCCM ili kuhakikisha kuwa  haki ya mtoto huyo inapatikana.
Awali akizungumza mara baada ya kukabidhiwa msaada wa baiskeli  ya magurudumu matatu na vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya shilingi laki saba na kamanda huyo, mama mzazi wa mtoto huyo Beatrice Kelvin,aliiomba serikali na wadau mbalimbali kujitokeza na kumsaida mwanae ili kuhakikisha haki inapatikana. 

Alisema kesi iliyokuwepo mahakama kwa ajili ya kudai haki za msingi za mwanae imeisha bila haki yake kupatikana licha ya kuhangaika sehemu mbalimba na kuomba vyombo husika vinavyo jishughulisaha na haki za binadamu kuingilia kati suala hilo hatua ambayo itasaida kupata haki.
                                                         Chanzo cha habari ni: Jiachie


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yatoa Ratiba Rasmi ya Uchaguzi Mkuu.

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ratiba rasmi kwa vyama vya Siasa na wananchi wote itakayotumika katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali  unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo  Jaji wa Rufaa (Mst.) Damian  Lubuva imesema kuwa kwa Mamlaka waliyopewa kwa mujibu wa vifungu vya 35B(1), (3) (a), 37 (1) (a) na 46 (1) vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,  Sura ya 343, shughuli za uchaguzi zinatarajia kuanza hivi karibuni.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa  Uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Udiwani unatarajia kufanyika Agosti 21, 2015, na  kampeni za Uchaguzi kwa wagombea hao zitatarajia kuanza Agosti 22 mpaka - Oktoba 24 mwaka huu.
Halikadhalika siku ya kupiga kura kwa wananchi wote inatarajiwa kuwa Oktoba 25, 2015 kwa wale waliojitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.
Chanzo ni Michuzi Jr

             MHE.MWIGULU NCHEMBA   AJIUZULU..SABABU KUBWA NI HII HAPA


Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba
----
Aliyekua Naibu Katibu Mkuu wa CCM -Bara,Mwigulu Nchemba amejiuzulu wadhifa huo.

Mwigulu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha,ametangaza kujiuzulu nafasu hiyo  jana Jioni katika kikao cha Halmashauri Kuu ya ya Taifa ya CCM,Mjini Dodoma

Akithibiths tukio hilo,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi ,Nape Nnauye amesema,Mwigulu ameamua kujiuzulu nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara kutokana na nia yake ya kutaka kuomba kuwania Urais kwa tiketi ya CCM  katika Uchaguzi utakaofanyika Octoba Mwaka huu

"Mwigulu alishamwambia nia hiyo Mwenyekiti wa Chama  Rais Jakaya Kikwete,nae Rais akamkubalia, na sasa  katika kikao ameomba rasmi kujiuzulu na Mwenyekiti Rais Jakaya Kikwete amemkubalia Mbele ya wajumbe wa NEC".amesema Nape

Nape amesema kufuatia uamuzi wa mwigulu  kujiuzulu, Mwenyekiti wa Chama Rais Jakaya Kikwete amemteua Msaidizi wake wa maswala ya siasa,Rajabu Ruhavi kuwa Mjumbe wa NEC na Wakati huohuo kamteua kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM -Bara Kushika nafasi iliyoachwa na Mwigulu Nchemba 
Chanzo ni Masama Blog

Monday, 2 February 2015

BREAKING NEWS..!! BONDIA FRANCIS CHEKA AHUKUMIWA JELA MIAKA 3 KWA KUMPIGA NGUMI MTU

Taarifa iliyoifikia Malunde1 blog hivi punde,inaenleza kuwa Bondia maarufu hapa nchini,Francis Cheka amehukumiwa kifungo cha Miaka mitatu (3) jela kwa kukutwa na hatia ya kumpiga na kumjeruhi Meneja wa Bar yake iliyopo mjini Morogoro.


Cheka alifikishwa kizimbani leo na kusomewa mashtaka ya kushambulia na kuzuru mwili,akidaiwa mnamo julai 02 mwaka 2014, bila uhalali na akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria, alimpiga kwa ngumi maeneo ya kichwani na tumboni, Bahati Kabanda maarufu kama Masika, na kumsababishia maumivu makali.

Hukumu hiyo imetolewa leo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi,Mkoani Morogoro.


Taarifa kamili itawajia baadae kidogo.

TOA MAONI YAKO HAPA

Sunday, 1 February 2015

KUWA WA KWANZA KUTAZAMA VIDEO MPYA YA DAVIDO "THE SOUND"....HII HAPA

. 
Staa wa Nigeria David Adedeji Adeleke aka Davido time amekuletea video ya single mpya inayoitwa The Sound akiwa amewashirikisha Dj Buckzpamoja na kundi la Uhuru kutokaea Afrika Kusini.
Itazame hapa #The Sound bonyeza play Hapo chini

TOA MAONI YAKO HAPA

MADAKTARI NA WAUGUZI WAUZA VIUNGO VYA MIILI YA WATOTO WALIOKUFA HOSPITALI KWA WAGANGA WA JADI!! A+A- PrintEmail

Wakati serikali ikihaha kutafuta muarobaini wa mauaji ya watu wenye ulemavu Ngozo (Albino),katika mikoa ya kanda ya ziwa,huku ikidiriki kutangaza vita dhidi ya wapiga ramli wote, katika hali isiyokuwa ya kawaida imebainika kuwa watoto ambao huzaliwa wakiwa hawajafikisha umri na kufa au kupoteza maisha wakati wa kuzaliwa viungo vyao huuzwa kwa waganga wa kienyeji katika hospitali ya wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.

Inaelezwa kuwa akina mama wanaojifungua watoto hao na kwa bahati mbaya kupoteza maisha, viungo vya watoto hao huwa havipelekwi kuzikwa kama ilivyo kawaida na taratibu za hospitali, badala yake wauguzi na wafanyakazi wengine huchukua viungo hivyo na kupeleka kwa waganga wa jadi.

Tuhuma hizo zilitolewa juzi mbele ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mwamvua Jilumbi katika kikao cha pamoja na wadau wa afya mkoa  kilichofanyika katika ukumbi wa kanisa la KKKT mjini Bariadi wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa kukomesha vifo vya wajawazito
na watoto mkoani Simiyu ulioko chini ya AMREF Tanzania.

Wadau hao walibainisha kuwa hali hiyo imekuwa ikijitokeza kila mara katika hospitali ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, ambapo walieleza kuwa mtandao mzima wa kuuzwa kwa viungo hivyo ufanyika kati ya wauguzi pamoja na madaktari ambao ndiyo wahusika wakuu kuzalisha akina mama wajawazito.

Mbele ya Katibu huyo tawala wa Mkoa wadau hao waliendelea kueleza kuwa viungo hivyo vimekuwa vikiuzwa kuanzia shilingi 400,000 hadi 500,000 kiasi ambacho walieleza hutolewa na waganga wa hao wa jadi.

“..katika hospitali yetu ya Bariadi kuna jambo ambalo siyo zuri na jema leo ngoja tulitoboe mbele ya kikao hiki na tena mbele za waandishi wa habari na wewe Katibu tawala wa Mkoa..akina mama wanaojifungua watoto wao kwa bahati mbaya akafariki viungo vya watoto hao huuzwa kwa waganga wa jadi” Alisema Gasper Mathew na kuongeza kuwa..

“ viungo hivyo vinauzwa shilingi 400,000 hadi 500,000 huu ni ushirikina wa hali ya juu na ni hatari..wauguzi pamoja na madaktari ndiyo wanahusika sana..wamekuwa wakipewa kiasi hicho..kila mara wanafaya hivyo lakini tumekuwa kimya” Alisema

Walisema kuwa akinamama  wengi hufika hospitalini hapo kwa lengo la kujifungua na mara wanapojifungua na kwa bahati mbaya mtoto au watoto kufariki  kutokana na matatizo ya afya ya uzazi baadhi huamua kuwahifadhi katika chumba cha maiti lakini wengi hujikuta wakirejea nyumbani mikono mitupu baada ya miili ya watoto wao kuuzwa kwa waganga wa kienyeji.

Akizungumzia tuhuma hizo Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,Mwamvua
Jilumbi katika kikao hicho alimtaka Mkurugenzi wa Halmshauri ya Mji wa Bariadi Erica Mssika kutoa maelezo juu ya tuhuma hizo.

Akitoa maelezo ya tuhuma hiyo Mkurugenzi huyo alisema kuwa hana taarifa yoyote juu ya kuwepo kwa vitendo hivyo katika hospitali yake, huku akieleza kuwa watafanya uchunguzi mara moja na watakao bainika kufanya hivyo watachukuliwa sheria mara moja.

“..hii ni hatari mimi hili nimelipata hapa na nimelisikia leo sina taarifa yeyote.. ila nawaomba wadau waliotoa tuhuma hizi tushirikiane tufanye uchunguzi haraka ili tuwabaini na watakaobainika tutawachulia sheria za kinidhamu” Alisema Mssika.

Katika kikao hicho Meneja Mradi wa Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na masula ya afya AMREF Health Africa tawi la Tanzania,katika mkoa wa Simiyu, Godfrey Matumu, aliitaka  jamii ya mkoa wa Simiyu kushiriki kikamilifu katika kuthibiti vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga wenye umri chini ya miaka mitano.

Alisema vifo hivyo  vimekuwa vikisababishwa na kuchelewa kupata huduma katika vituo vya afya kwa wakati.wakati wa kuzindua Mpango Mkakati wa Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto katika mkoa wa Simiyu utakaotekelezwa kwa muda wa miaka 4 (2014-18),chini ya msaada wa watu wa Canada.
Chanzo-http://simiyunews.blogspot.com

TOA MAONI YAKO HAPA

KIMBUNGA CHALETA MAAFA BUKOBA.....WAWILI WAFARIKI, 31 WALAZWA NA 380 HAWANA MAKAZI


Watu wawili wamefariki dunia baada ya kimbunga kupiga katika Kisiwa cha Goziba na kusababisha baadhi ya mitumbwi kupinduka katika Ziwa Victoria.


Kimbunga hicho kilitokea juzi saa tano asubuhi wakati wakazi mbalimbali wakiwa katika shughuli zao.
 

Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Rembris Kipuyo alisema jana kuwa, majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera.
 

Alisema kimbunga hicho hakikuwa cha kawaida kwa kuwa kiliharibu nyumba na zaidi ya mitumbwi arobaini imepotea.
 

Miongoni mwa walionusurika, Mariagoreth Phares alisema tukio hilo lilikuwa kama muujiza kwa kuwa aliona kitu kilichosogea kutoka angani.
 

Alisema nyumba zilianza kung’olewa kwa upepo na watu kurushwa majini, huku wengine wakipoteza fahamu.
 

Alisema baadhi ya watu walikuwa wakijaribu kujiokoa kwa kutambaa ili wasipigwe na vitu vilivyokuwa viking’olewa na kurushwa na upepo.
 

Majeruhi mwingine Leah Lazaro alisema aliona kitu kilichokuwa kinachemsha maji kwa kasi ziwani kuelekea kwenye kisiwa hicho.
 

“Nilikuwa mwaloni nikaona kitu kinachemsha maji kwa kasi nilikimbia na kumkumbatia mtoto wangu ambaye aliniponyoka,” alisema Lazaro.
 

Kisiwa cha Goziba kipo umbali wa kilomita 80 kutoka Wilaya ya Muleba na kipo karibu zaidi na Mkoa wa Mwanza.
 

Wakazi wa kisiwa hicho hupata mahitaji yao Mwanza. Kipuyo alisema baada ya kamati ya maafa kutembelea eneo hilo, itatoa tathimini ya kiwango cha hasara kilichotokea.


Aliwaomba wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia wakazi wa kisiwa hicho ambao wengi wao wamepoteza mali.
Habari na Masamablog.com

TOA MAONI YAKO HAPA